Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Video ya ngono ya Waziri yavuja, aomba radhi
Kimataifa

Video ya ngono ya Waziri yavuja, aomba radhi

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba yuko katika wakati mgumu baada ya video ya ngono iliyomhusisha yeye na mkewe kuvuja mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika utetezi wake kupitia akaunti yake ya Twitter, jana aliandika kuwa, video hiyo imevujishwa na wahalifu wa mtandaoni walio ingilia simu yake, huku akidai kwamba ni miongoni mwa mashambulizi ya kisiasa yaliyoanza kuibuka tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Fedha Machi 31, 2017.

Gigaba amejitetea kuwa, alijirekodi video hiyo kwa ajili ya matumizi yake binafsi lakini imesambazwa na wahalifu baada ya mawasiliano yake kuingiliwa.

“Mke wangu na mimi tumejifunza, tumejutia na kuhuzunika kuona kwamba video ya ngono ambayo ilikuwa kwa ajili ya macho yetu imeibiwa wakati mawasiliano yangu yameingiliwa. Nachukua fursa hii kuomba msamaha kwa umma na familia yangu hasa watoto wangu, mama yangu, mkwe wangu kwa maumivu na aibu kufuatia video hii iliyosambazwa mitandaoni,” aliandika Gigaba Twitter.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!