Wednesday , 6 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Video ya ngono ya Waziri yavuja, aomba radhi
Kimataifa

Video ya ngono ya Waziri yavuja, aomba radhi

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba yuko katika wakati mgumu baada ya video ya ngono iliyomhusisha yeye na mkewe kuvuja mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika utetezi wake kupitia akaunti yake ya Twitter, jana aliandika kuwa, video hiyo imevujishwa na wahalifu wa mtandaoni walio ingilia simu yake, huku akidai kwamba ni miongoni mwa mashambulizi ya kisiasa yaliyoanza kuibuka tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Fedha Machi 31, 2017.

Gigaba amejitetea kuwa, alijirekodi video hiyo kwa ajili ya matumizi yake binafsi lakini imesambazwa na wahalifu baada ya mawasiliano yake kuingiliwa.

“Mke wangu na mimi tumejifunza, tumejutia na kuhuzunika kuona kwamba video ya ngono ambayo ilikuwa kwa ajili ya macho yetu imeibiwa wakati mawasiliano yangu yameingiliwa. Nachukua fursa hii kuomba msamaha kwa umma na familia yangu hasa watoto wangu, mama yangu, mkwe wangu kwa maumivu na aibu kufuatia video hii iliyosambazwa mitandaoni,” aliandika Gigaba Twitter.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!