MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) nchini Tanzania imetoa mafunzo na vyeti kwa vijana zaidi ya 10,000 nchi nzima wenye ujuzi nje ya mfumo rasmi wa kupitia mamlaka hiyo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Hayo yamebainishwa na Afisa Uhusiano VETA, Dorah Tesha alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafunzo na mikakati inayofanywa na chuo hicho sambamba na kuwarasimisha vyeti vya ujuzi vijana ambao wamepata ujuzi nje ya mfumo rasmi.
Dorah akiwa katika maonesho ya elimu ya ufundi shindani yanayoratibiwa na (Nactvet) na kueleza kwa sasa vyuo vya VETA vimejengwa 40 nchi nzima na ujenzi wa vyuo kila wilaya unaendelea.
Aidha, amesema kutokana na vijana wengi kupata ujuzi mitaani bila kupitia vyuo vya VETA kwa kushirikiana na ofisi ya waziri mkuu walianzisha kitengo cha kupitia maeneo mbalimbali na kuweza kutoa elimu kwa vijana hao na kuwapatia vyeti vya ujuzi ili kuweza kuwafanya waweze kupata ajira za uhakika au kupata tenda kadri ya kile anachokijua.
“Serikali iliona wapo vijana wengi ambao wanaujuzi wa kufanya shughuli mbalimbali lakini hawana vyeti hivyo hawawezi kuomba kazi popote wakapata.”
“Kutokana na hali hiyo VETA kwa kushirikiana na ofisi ya waziri mkuu ilianzisha utaratibu wa kupita kwenye magereji pamoja na sehemu mbalimbali na kutoa mafunzo kwa vijana ambao wamekuwa na ujuzi nje ya mfumo rasmi kwa zaidi ya miaka mitano na kuwarasmisha vyeti vya ufundi,” amesema
“Kutokana na mkakati huo zaidi ya vijana 10,000 wamerasimishwa vyeti vya ujuzi kutoka VETA na kwa kufanya hivyo tayari vijana hao kwa sasa wanaweza kuajiriwa, kuomba zabuni yoyote kulingana na ujuzi wa mtu alionao,” amesema
Aidha, afisa huyo amesema nafasi za kuwapata mafunzo na vyeti vijana ambao wanaujuzi nje ya mfumo rasmi utolewa kila baada ya miezi mitatu na mafunzo hayo utolewa bure kwani ugharamiwa na serikali.
Pamoja na mambo mengine, Dorah amesema VETA itoa mafunzo ya aina yoyote ya ufundi ambayo umwezesha mtu yoyote kuweza kujiajiri au kuajiriwa na kueleza mafunzo hayo utolewa kwa muda mfupi na muda mrefu.
Leave a comment