Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Veta yaanzisha kozi ya makanikia
ElimuHabari Mchanganyiko

Veta yaanzisha kozi ya makanikia

Yona Mwambopa, Mkufunzi wa Veta akizungumza na Mwandishi wa habari wa MwanaHALISI Online katika viwanja vya Sabasaba
Spread the love

CHUO cha Ufundi Stadi (VETA) kimeanzisha kozi itakayozalisha wahitimu watakaosaidia kuchakata na kung’arisha madini ya vito, anaandika Jovina Patrick.

Kozi hiyo inakuja kipindi ambacho hivi karibuni serikali imezuia kusafirisha mchanga wa madini (makinikia) nje ya nchi ili kuuchakata.

Akizungumza kuhusu kozi hiyo, Yona Mwambopa Mkufunzi wa Veta, amesema kozi hiyo kwa mara ya kwanza waliitambulisha miaka mitatu iliyopita ila ikakabiliwa na changamoto za kutokuwa na vitendea kazi vya ufundishaji.

“Kama tungekuwa na vifaa tayari tungekuwa tumeshazalisha wataalam wetu hapa hapa nchini,” amesema Mwambopa.

Mwambopa amesema kwamba mwaka huu wameanzisha tena kozi hii lakini muitikio sio wa kuridhisha.

“Hadi sasa tuna wanafunzi 12 ambao wapo chini ya kadirio la elimu nchini wakati inahitaji wanafunzi wasiopungua 16 na wasiyozidi 20,” amesema.

Amesema sababu ya muitiko kuwa mdogo umetokana na ugeni wa kozi hiyo wengi hawajafahamu faida zake, kwani Watanzania wengi wamekuwa wakisoma kozi baada ya kujua faida wanayopata baada ya kuhitimu.

Mwambopa anasema: “Naamini baada ya mafanikio yatakayopatikana kwa wahitimu hawa itawavutia wengine kujiunga zaidi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!