Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa UWT wamwangukia Rais Samia
Habari za Siasa

UWT wamwangukia Rais Samia

Katibu Mkuu wa UWT, Dk. Phillis Nyimbi
Spread the love

 

UMOJA wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), umemuomba Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, atatue changamoto zinazoukabili, ikiwemo ukosefu wa mitaji ya kuendeleza miradi yake na uchakavu wa vifaa vya usafiri. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani … (endelea).

Ombi hilo limetolewa leo Jumamosi, tarehe 23 Oktoba 2021 na Katibu Mkuu wa UWT, Dk. Phillis Nyimbi, katika maadhimisho ya kilele cha wiki ya umoja huo, yaliyofanyika wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani.

“Pamoja na mafanikio mazuri na shughuli tunazofanya, tukiendelea kuwa jumuiya ndani ya CCM, jumuiya yetu inakabiliwa na changamoto angalau hizi naomba nitumie fusra hii kuzieleza. Tuna uhaba au upunfufu wa mitaji wa kuweza kuendeleza miradi mikubwa,” amesema Dk. Nyimbi.

Dk. Nyimbi amesema “ tuna maono mazuri ndani ya jumuiya tunakwama kwenye suala la mitaji, lakini tunaendelea kupanua wigo vyanzo vyetu vya mapato. Tukusanye tuelete chachu ya mapinduzi ya kiuchumi ndani ya jumuiya yetu.”

Kuhusu changamoto ya uchakavu wa vifaa vya usafiri, Dk. Nyimbi amesema inakwamisha shughuli za jumuiya hiyo kwa kuwa vinahitaji marekebisho ya mara kwa mara.

“Tunao upungufu wa vitendea kazi, vyombo vya usafiri tunavyoitumia ni vya muda mrefu vinatumia marekebisho makubwa, ukiachilia kwamba vimechoka. Hii ni changamoto yetu na muda mwingine inapelekea kwenye speed kuchelewa kidogo,” amesema Dk. Nyimbi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!