Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko UWT Kivukoni Dar waadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa kupima afya bure
Habari Mchanganyiko

UWT Kivukoni Dar waadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa kupima afya bure

Spread the love

UMOJA wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi UWT Kata ya Kivukoni jijini Dar es Salaam umeadhimisha Siku ya Wanawake duniani kwa kuendesha kampeni ya upimaji afya bure kwa wanawake wa jiji la Dar es Salaam, ikiwa ni ishara ya kuthamini afya ya mwanamke katika maendeleo ya Taifa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kivukoni Mariam Kimbisa akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya upimaji afya kwa wanawake, Karimjee jijini Dar es Salaam

Uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika  juzi tarehe 8 Machi 2023 katika viwanja vya Karimjee, uliwavuta wanawake wengi waliofika kupima afya zao na kukutana na watalaamu mbalimbali wa masuala ya afya huku mgeni rasmi katika hafla hiyo akiwa ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapunduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu.

Huduma zilizotolewa ni pamoja na upimaji wa saratani ya matiti na kizazi, magonjwa ya moyo, kisukari, macho, meno, ushauri kuhusu lishe na uhamasishaji wa bima ya afya kwa wanawake.

Akizungumza kabla ya uzinduzi wa kampeni hiyo Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kivukoni, Mariam Kimbisa alisema wameamua kuadhimisha Siku ya Mwanamke duniani kwa upimaji wa afya, kwa kuwa UWT Kata ya Kivukoni inaamini afya ndiyo mtaji katika shughuli za maendeleo na kueleza kampeni hiyo ni endelevu itakuwa ikifanyika kila mwaka Machi 8.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es salaam Abbas Mtemvu akimpongeza Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kivukoni Mariam Kimbisa kwa niaba ya umoja wa wanawake kata kwa kampeni hiyo ya afya

“Wanawake ni jeshi kubwa, sisi UWT Kata ya Kivukoni tunayofuraha kubwa ya kumshukuru Mwenyekiti wetu wa chama Mkoa wa Dar es Salaam ndugu Abbas Mtemvu ambaye amekuja kujumuika nasi na kutuunga mkono katika kampeni hii muhimu katika kuadhimisha siku ya mwanamke duniani

“Katika kutambua siku ya wanawake duniani UWT Kata ya Kivukoni tumeamua kuadhimisha siku hii kwa kutoa huduma ya afya bure kwa akina mama. Tunatumia siku hii kuhamasisha wanawake kutambua umuhimu wa afya bora na vile vile upatikanaji wa huduma za fya bora

“Hii inawezekana kwa kila mwanamke kuwa ana afya bora tukiunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais wetu mpendwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikiha wanawake wote nchini wanapata huduma bora ya afya, kwani ukimponya mwanamke umeponya taifa, alisema Mariam.

Machi 8 kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya Wanawake, ambapo katika siku hii, wanawake wanakutana na kujadiliana kuhusu mafanikio waliyopata katika sekta mbalimbali, changamoto wanazopitia na jinsi ya kukabiliana nazo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!