Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Uvamizi Segerea’: Mdee, Bulaya waanza kusota Kisutu
Habari za Siasa

‘Uvamizi Segerea’: Mdee, Bulaya waanza kusota Kisutu

Spread the love

HALIMA Mdee, Mbunge wa Kawe na wenzake 14, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kufanya vurugu katika gereza la Segerea. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).   

Kwenye kundi hilo, wapo wajumbe wanne wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), pamoja na wanachama 10 wa chama hicho.

Bmali na Mdee, wengine ni Esther Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini; Jesca Kishoa, Mbunge Viti Maalumu; Boniface Jacob, Meya wa Ubungo na Henry Kilewo, mjumbe wa kamati hiyo, wamefikishwa mahakamani hapo leo tarehe 23 Machi 2020.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema katika ukurasa wake wa Twitter, watuhumiwa hao walitakiwa kuripoti polisi leo, lakini wamepelekwa mahakamani.

Mdee na wenzake wanatuhumiwa kufanya fujo katika Gereza la Segerea, walipokwenda kumtoa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema, aliyekuwa anatumikia kifungo cha miezi mitano gerezani hapo.

Kwa mujibu wa Chadema, hadi sasa watuhumiwa hao hawajapandishwa kizimbani.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE kwa taarifa zaidi…

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!