Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Utatuzi Masheikh wa Uamsho wanukia
Habari za Siasa

Utatuzi Masheikh wa Uamsho wanukia

Spread the love

 

OTHMAN Masoud Othman, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, ameahidi kuendelea juhudi zilizofanywa na mtangulizi wake Hayati Maalim Seif Shariff Hamad na rais wa sasa wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi kuhusu masheikh wa Uamsho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Akizungumza katika Msikiti wa Maghfira, Unguja Ijumaa tarehe 16 Aprili 2021, Othman amesema atashirikiana na Rais Mwinyi katika juhudi hizo.

Masheikh wanaoshikiliwa kwa tuhuma za ugaidi ni Farid Hadi Ahmed, Hamisi Salum, Saidi Amour Salum, Anthari Ahmed, Amir Hamis Juma, Abdallah Hassan, Alawi Amir, Mohammed Yusuph, Sheikh Mselem Ali Mselem na Said Sharifu.

Wengine ni Juma Juma, Hassan Suleiman, Salum Ali Salum, Abdallah Said Ali, Hussein Ally, Kassim Nassoro, Abubakar Mngodo, Rashid Nyange, Jamal Swalehe, Nassoro Abdallah, Saidi Ally na Salum Amour Salum.

Othman Masoud Othman, Makamu wa Kwanza wa Zanzibar

Othman amesema, Maalim Seif wakati wa uhai wake, alishirikiana vizuri na Rais Mwinyi katika kuliangaliajambo hilo, na kwamba ataendelea pale alipoishia mtangulizi wake (Maalim Seif), aliyefariki dunia tarehe 17 Februari 2021.

“Wakati wake (Maalim Seif) alishirikiana vizuri na Rais Mwinyi. Walifanya juhudi kubwa kuhakikisha suala la masheikh wa Uamsho linapatiwa ufumbuzi, juhudi hizo zimefika pazuri. Nitaendelea kuungana na Rais Mwinyi kupatia ufumbuzi suala hilo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!