Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Utabiri wa MwanaHALISI, watimia, Mbunge wa Chadema ang’oka
Habari za SiasaTangulizi

Utabiri wa MwanaHALISI, watimia, Mbunge wa Chadema ang’oka

Spread the love

MBUNGE wa Chadema katika jimbo la Siha, mkoani Kilimanjaro, Dk. Godwin Mollel, amekihama chama hicho. Anaripoti Pendo Omary…(endelea).

Dk. Mollel alitangaza kujivua uanachama wa chama hicho leo mchana kupitia taarifa kwa umma na video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Dk. Mollel alisema, amechukua uamuzi huo akiwa na akili timamu kwa lengo la kumuunga mkono Rais John Pombe Magufuli.

 

MwanaHALISI liliandika mwezi mmoja uliopita kuwapo kwa mkakati wa wabunge wawili, mmoja kutoka Chadema na mwingine kutoka Chama cha Wananchi (CUF).

Tayari mbunge wa Kinondoni kupitia CUF ametangaza kujiuzulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

error: Content is protected !!