Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ushuru bidhaa ya bia kupunguzwa 2021/22
Habari MchanganyikoTangulizi

Ushuru bidhaa ya bia kupunguzwa 2021/22

Spread the love

 

WAZIRI wa Fedha na Mipango Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba amependekeza kufanya ushuru wa bidhaa ikiwemo bia kuanzia mwaka wa fedha 2021/22. Anaripoti Jemima Samwel, DMC…(endelea).

Akiwasilisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2021/22, bungeni jijini Dodoma, leo Alhamisi, tarehe 10 Juni 2021, Dk. Mwigulu amesema “kupunguza ushuru wa bidhaa kwenye bia zinazotengenezwa kwa kutumia shayiri iliyozalishwa hapa nchini kutoka Sh.765 kwa lita za sasa hadi Sh.620 kwa lita.”

amesema “lengo la mapendekezo haya ni kuchochea kilimo cha shayiri hapa nchini.”

Amesema, kuanza kutoza Ushuru wa bidhaa wa asilimia 10 kwenye nyuzi na kamba za plastiki (synthetic fibres) zinazoingizwa kutoka nje ya nchi au kuzalishwa hapa nchini zinazotambuliwa kwa heading 55.11 na 56.07 isipokuwa zile zinazotumika kwenye Uvuvi (HS Code 5607.50.00).

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Dk. Mwigulu amesema, lengo la marekebisho haya ni kulinda mazingira na kuchochea uzalishaji na matumizi ya bidhaa za katani. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa Sh.2,644 milioni.

Waziri huyo amesema, kuanzisha tozo ya ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha asilimia 10 kwenye pikipiki zilizotumika kwa zaidi ya miaka 3 zinazoingizwa nchini zinazotambuliwa kwa HS Code 8711.

“Lengo la marekebisho haya ni kudhibiti uingizaji wa pikipiki chakavu na kulinda mazingira. Hatua hii inatarajiwa kuongeza ya mapato ya Serikali kwa Sh.263.7 milioni,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!