UONGOZI wa timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam nchini Tanzania imewashukuru mashabiki kwa kuchagiza ushindi wa 3-1 wa dhidi ya Asec Mimosas ya Ivory Coast kwenye mchezo wa makundi wa Kombe la Shirikisho Afrika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Simba iliibuka na ushindi huo mkubwa jana Jumapili, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Magoli hayo yalifungwa na Pape Sakho, Shomari Kapombe kwa penati pamoja na Peter Banda.
Taarifa ya Simba iliyotolewa leo Jumatatu, tarehe 14 Februari 2022 imewaomba mashabiki zao kutowasumbua mashabiki wengine wanaofika uwanjani kushuhudia michezo yao.
“Ukweli ni kwamba mashabiki wa timu nyingine wanakuja kwenye mechi zetu kufuata burudani ambayo hawaipati kwenye timu zao hivyo ni vema kuwapokea na kuwapa mazingira mazuri ya kufurahia kabumbu safi kutoka Simba,” imeeleza taaifa hiyo.
Leave a comment