JOSEPH Butiku, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku amewataka wanasiasa nchini kusimamia haki kwa kuwa utu na usawa pekee havitoshi. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Akizungumza kwenye mkutano wa Chama cha NCCR-Mageuzi, uliofanyika kwa lengo la kuchagua viongozi wapya wa chama hicho tarehe 27 katika ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dae rs Salaam, amesema inahitajika unyenyekevu kusimamia amani.
“Usawa na utu hautoshi, lazima kuwe na haki maana kila mtu anastahili haki, msingi huo ndio unatawala vyama vyetu vyote,” amesema Butiku akisistiza kwamba “tukifanya hayo, tutapata amani.”
Mwanasiasa huyo mkongwe nchini, amesema vyama vinapaswa kuwa na utaratibu wa kujifunza kutoka kwenye vyama vingine, na kwamba jambo hilo linaweza kusaidia kuendeleza Amani iliyopo sasa.
“Ninashukuru mmepata nafasi ya kutuita hapa na ninawaombea muendelee hivyo, Mbatia huwa ninakuangalia huwa unasema mambo mengi ya busara hivyo ongoza chama hiki kiwe cha busara na kisaidiane na chama tawala nacho kijifunze,” amesema.
“Mimi ninajifunza kwenu miaka yangu 81 ninawafundisha na kujifunza pia, ninyi vyama mlivyotangulia na vilivyozaliwa jengeni uwezo kwa kujifunza miongoni mwenu, CCM mjifunze kwa vingine na ninyi mjifunze kutoka kwao pia na mfanye hivyo kwa unyenyekevu,” amesema.
Aidha amesisitiza vijana kuwa na utu kwakua ndio msingi wa Taifa la Tanzania ambapo amesema iwapo kutakuwa na utu, usawa na na haki nchi itakuwa na amani.
“Ninawakumbusha vijana taifa hili wakati linaasisiwa msingi wake ulikua ni utu na usawa wa utu ukikataa hilo maana yake unakataa utu kwasababu mwenzako nae anaweza akakukataa,” amesema.
Leave a comment