Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Michezo Usain Bolt asaini Mamelods ya Afrika Kusini
Michezo

Usain Bolt asaini Mamelods ya Afrika Kusini

Usain Bolt (katikati) akikabidhiwa jezi namba moja atakayoitumia akiwa na kikosi hicho
Spread the love

BAADA ya Mwanariadha Usain Bolt wa Jamaika kutamba katika mbio fupi duniani na kuweka rekodi kadhaa ameamua kugeukia mchezo wa soka baada ya kusaini kandarasi ya kuichezea klabu ya Mamelods Sundowns ya nchi Afrika ya Kusini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bolt ambaye ndiye binadamu mwenye kasi zaidi duniani alikuwa na ndoto ya kucheza soka muda mrefu huku akitajwa mara kadhaa kutaka kuichezea klabu ya Manchester United.

Wadau wengi wa soka wanasubiri kuona uwezo aliouonyesha katika medani ya riadha katika mbio za mita 100 na 200 atauhamishia katika soka ndani ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini na michuano ya kimataifa ambayo timu yake mpya itashiriki.

Bolt amekabidhiwa jezi namba moja iliyozoeleka kutumiwa na makipa, lakini akiwa katika klabu hiyo ataitumia akiwa mchezaji wa ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!