Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi yampa uraia Edward Snowden
Kimataifa

Urusi yampa uraia Edward Snowden

Edward Snowden
Spread the love

 

RAIS wa Urusi, Vladimir Putin amempa uraia kachero na mhandisi wa zamani wa Marekani, Edward Snowden, ambaye tangu mwaka 2020 amekuwa mkaazi wa kudumu nchini Urusi.

Dikrii iliyotolewa jana tarehe 26 Septemba, 2022 na Rais Putin, iliwapa uraia wa Urusi raia 72 wa kigeni.

Licha ya kwamba haifahamiki iwapo Snowden ameukana uraia wake wa Marekani, kachero huyo aliyetuhumiwa kuvujisha siri za Taifa hilo, anatakiwa nchini Marekani kukabiliana na mashtaka ya ujasusi.

Mfanyakazi huyo wa zamani wa Shirika la Usalama la Marekani aliikimbia nchi hiyo baada ya kuvujisha nyaraka za programu za ujasusi mwaka 2013.

Alikuwa ameshafanyia kazi shirika hilo tangu mwaka 2009. Mwaka 2019, Snowden alisema alikuwa tayari kurejea Marekani ikiwa angelihakikishiwa kutendewa haki kwenye kesi dhidi yake.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Marekani, Ned Price, amesema msimamo wa Marekani juu ya Snowden haujabadilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!