Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi imelipua bwawa kuu la umeme nchini Ukraine
Kimataifa

Urusi imelipua bwawa kuu la umeme nchini Ukraine

Spread the love

SERIKALI mjini Kyiv nchini, Ukraine imeushutumu utawala wa Rais Vladimir Putin wa Urusi, kwa kulipua bwawa lake kubwa katika kituo cha kuzalisha umeme kwa njia ya maji kwenye mto Dnipro, katika eneo la Kherson kusini mwa nchi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, kwa msaada wa mitandao ya kijamii….(endelea).

 Bwawa hilo liko katika mji wa Nova Kakhovka, unaokaliwa kwa mabavu na Urusi, ambapo meya aliyewekwa na Moscow ameilaumu Ukraine kwa uharibifu huo.

Hata hivyo, meya huyo anasema, “ni sehemu ya juu ya mtambo pekee ndiyo iliyoharibiwa na makombora; na wala siyo bwawa lenyewe.”

Lakini jeshi la Ukraine limevishutumu vikosi vya Urusi kwa kulipua bwawa hilo kubwa, huku kukiwa na hofu kwamba maelfu ya nyumba zilizo chini ya mto huo sasa zitafurika. Hakuna vyanzo huru vya kuthibitisha madai hayo.

Taarifa ya jeshi la Ukraine inasema, “linachunguza kiwango cha uharibifu.”

Bwawa hilo – Kakhovska (HPP), lililojengwa ya zama za umoja wa Soviet – liko katika mji wa Nova Kakhovka, katika mkoa wa Kherson nchini Ukraine.

Jiji na maeneo mengine kwenye ukingo wa kushoto ya mto Dnipro (mashariki) kwa sasa, yanashikiliwa na Urusi.

Mfereji muhimu wa kubeba maji kutoka Dnipro hadi Crimea inayokaliwa na Urusi, unaoanzia Nova Khakovka, una uwezekano wa kuathirika, pamoja na kituo cha nishati ya nyuklia huko Zaporizhzhia, ambacho kiko kwenye ukingo wa Dnipro karibu kilomita 160 juu ya mto.

Katika taarifa yake asubuhi ya leo, Andryi Yermak, mkuu wa ofisi ya Rais Zelensky, alisema kuwa Urusi itawajibikia kuwanyima maji ya kunywa watu wa Crimea na kuongeza kuwa vitendo vya Urusi “vinatishia ZNPP” (kinu cha nyuklia cha Zaporizhzhia).

Huku hayo yakijiri, habari zaidi zinasema Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameitisha mkutano wa dharura wa baraza la usalama na ulinzi la taifa la nchini mwake.

Oleksiy Danilov, ambaye ni katibu wa baraza hilo, alisema kwenye Twitter, kwamba mkutano huo ulikuwa unafanyika “kuhusiana na mlipuko wa bwawa la Kakhovsky.”

Taarifa za hivi punde zinasema, maji yanafurika kwenye mto Dnipro na inasemekana yanatishia kusababishia mafuriko makubwa mjini Kherson.

Shughuli ya uokoaji inafanyika katika eneo hilo huku watu wasiopungua 16,000 wakiwa hatarini kutokana na mafuriko hayo, gavana wa Ukraine amesema.

Kinu cha nyuklia cha Zaporizhzhia kinategemea maji ya mto huo kupoza vinu vyake. Hali ya huko kwa sasa inasemekana kudhibitiwa. Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), linasema linafuatilia kwa karibu sakata hilo.

Wakazi katika maeneo yaliyo lwenye hatari wanahamishwa kwa mabasi hadi Kherson, kisha watahamishwa hadi miji tofauti nchini kote ikiwa ni pamoja na mji mkuu, Kyiv, Prokudin anasema katika chapisho la telegram.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!