Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Upinzani washinda uchaguzi DRC, Kabila chali
Kimataifa

Upinzani washinda uchaguzi DRC, Kabila chali

Felix Tshisekedi, Rais wa DR Congo
Spread the love

MGOMBEA wa upinzani, Felix Tshisekedi wa Chama cha UDPS ameshinda uchaguzi wa urais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), tume ya uchaguzi imesema. Vinaripoti vyombo vya kimataifa….(endelea).

Matokeo ya awali yanaonyesha mgombea huyo wa upinzani amemshinda mgombea mwingine wa upinzani Martin Fayulu, pamoja na mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na serikali Emmanuel Shadary.

Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Ceni) Corneille Nangaa, alisema mapema Alhamisi kwamba Tshisekedi alipata asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa na “anatangazwa mshindi wa urais mteule.”

Tshisekedi alipata zaidi ya kura milioni saba 7 huku Fayulu akapata kura takriban 6.4 milioni na mgombea anayeungwa mkono na serikali, Emmanuel Ramazani Shadary akipata takriban kura 4.4 milioni.

Tayari tume ya uchaguzi imemtangaza mpinzani kushinda uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Kimataifa

Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini China chaongezeka

Spread the love  WAKATI kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...

Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Spread the love OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa...

error: Content is protected !!