Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Upinzani wapata pigo DRC
Habari za SiasaKimataifa

Upinzani wapata pigo DRC

Etienne Tshisekedi kiongozi wa chama cha upinzani cha (UDPS)
Spread the love

KIFO cha Etienne Tshisekedi kiongozi wa chama cha upinzani cha (UDPS) katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kimeacha simanzi na pigo kwa wapenda mageuzi nchini humo, anaandika Wolfram Mwalongo.

Tshisekedi aliyekuwa na umri wa miaka 84 amefariki dunia akiwa mjini Brussels, Ubelgiji alipokuwa akipatiwa matibabu ingawa hadi sasa tarifa za ugonjwa uliokuwa ukimsumbua hazijawekwa wazi.

Taarifa hizo zimenyong’onyeza wapinzani nchini Kongo huku baadhi wakiamini kwamba kuondokewa na kiongozi huyo ni pigo kubwa katika mapambano ya kutetea demokrasia katika taifa hilo lenye historia ya vita za wenyewe kwa wenyewe.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba, enzi za uhai wake Tshisekedi alikuwa mstari wa mbele kupinga waziwazi ukiukwaji wa haki za binadamu, ukandamizaji wa demokrasia na ufisadi.

Mbali na kuwa mkosoaji mkubwa wa utawala wa Rais king’ang’anizi madarakani, Joseph Kabila lakini pia kiongozi huyo aliwahi kushika nafasi mbalimbali wakati wa utawala wa Mobutu Sese Seko kabla ya kujiuzulu waliposhindwa kuafikiana katika maamuzi aliyodai yanakandamiza wananchi.

Taarifa zaidi kutoka nchini Kongo zinadai kuwa kiongozi huyo alikuwa akitarajiwa kushika nafasi ya juu ya uongozi katika serikali ya muungano ambayo ingeundwa baina ya wapinzani na Rais Kabila hadi pale uchaguzi mkuu utakapofanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

error: Content is protected !!