MAWAZIRI watatu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao ni wanachama wa chama cha mgombea urais, Moise Katumbi wamejiuzulu leo tarehe 29 Disemba, 2022 baada ya rais wa nchi hiyo kutaka kufahamu ni nani wangemuunga mkono katika uchaguzi ujao. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Katumbi (57) – mfanyabiashara tajiri ambaye aliwahi kuongoza eneo lenye utajiri wa madini la Katanga, mapema mwezi huu alitangaza kwamba atagombea nafasi ya rais katika uchaguzi uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka 2023.
Rais Felix Tshisekedi aliwaita leo mawaziri watano ambao ni wanachama wa chama cha Katumbi cha Ensemble pour la Republique ili kujua msimamo wao na ndipo Waziri wa mipango, waziri wa uchukuzi na naibu waziri wa afya walipowasilisha baadaye ombi lao la kujiuzulu.
Tshisekedi, ambaye aliingia madarakani Januari mwaka 2019, tayari ametangaza kuwa ana nia pia ya kugombea muhula wa pili mwaka ujao.
Leave a comment