Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Upepo, mvua kubwa, mawimbi: TMA yatoa tahadhari
Habari Mchanganyiko

Upepo, mvua kubwa, mawimbi: TMA yatoa tahadhari

Moja ya sehemu za Jiji la Dar es Salaam lililoathirika na mvua zinazoendelea kunyesha
Spread the love

MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini (TMA), imewataka wananchi kuchukua tahadhari kutokana na kuwepo kwa vipindi vifupi vya mvua kubwa, upepo mkali na mawimbi makubwa, vinavyotarajiwa kujitokeza katika baadhi ya maeneo nchini. Anaripoti Martin Kamote…(endelea).

Pia, imewataka wananchi kuendelea kufuatilia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na mamlaka hiyo, ili kuweza kuwa na habari sahihi kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa nchini.

Dk. Agnes Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa TMA amesema, wahati huu wa mvua za vuli, inatarajiwa kuwepo vipindi vifupi vya mvua kubwa na kwamba, mvua zinazoendelea kwa sasa, ni za msimu wa vuli kwa maeneo yanayopata mvua mbili kwa mwaka.

Akieleza utaratibu wa mvua kwa Novemba 2019 hadi Aprili 2020 amesema, wananchi wa mikoa ya Kigoma, Tabora,Rukwa, Katavi, Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa, Lindi, Dodoma, Singida, Mtwara na Kusini mwa Mkoa wa Morogoro yanatarajiwa kuwa na mvua za kutosha.

“Wananchi wa maeneo hayo wanapaswa kuzitumia vizuri mvua hizo kwa kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa sekta husika, kwa vile maeneo mengi yanatarajiwa kuwa na mvua za kutosha,” amesema na kuongeza:

“Naendelea kutoa rai kwa wananchi wa mikoa husika kuzitumia mvua hizi kwa kupanda mazao sahihi kwa kufuata ushauri wa wataalamu, kama tunavyoona maeneo mengi yatarajiwa kuwa na mvua za juu ya wastani hadi wastani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yatoa msaada wa mil. 20 kwa waathirika mafuriko Hanang

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) sambamba na wafanyakazi wa...

Habari Mchanganyiko

Polisi wadaka mirungi kwenye basi la Extra Luxury

Spread the loveJeshi la polisi mkoani Kilimanjaro limekamata shehena ya dawa za...

Habari Mchanganyiko

Oryx yaungana na jamii kuwafariji waathirika maporomoko Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeungana na Watanzania kutoa pole...

Habari Mchanganyiko

Amsons Group watoa milioni 100 waathirika maafa Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...

error: Content is protected !!