Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Upelelezi wa Lowassa bado pasua kichwa
Habari za SiasaTangulizi

Upelelezi wa Lowassa bado pasua kichwa

Edward Lowassa alipowasili Makao Makuu wa Jeshi la Polisi
Spread the love

JESHI la Polisi Tanzania bado halijakamilisha upelelezi wa tuhuma zinazomkabiri Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, hivyo wamelazimika kumwachia na kumtaka arudi tena baada ya wiki tatu, anaandika Mwandishi Wetu.

Lowassa aliwasili Makao Makuu ya Polisi saa mbili asubuhi kama alivyoagizwa wiki iliyopita na kuingia moja kwa moja kwenye ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Boaz.

Waziri Mkuu huyo wa zamani aliambatana na mkewe, Regina na mwanasheria wake, Peter Kibatala.

https://youtu.be/YnLYXHocwRo

Muda mchache mara baada ya kuwasili, Lowassa alipewa maelekezo kuwa upelelezi haujakamilika hivyo aliruhusiwa kuondoka na kutakiwa kurudi tena kwa DCI baada ya wiki.

Leo ni mara ya nne kwa Lowassa kuripoti hapo akituhumiwa kutoa kauli za kichochezi wakati wa futari iliyoandaliwa Juni 23, na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.

Katika futari hiyo, Lowassa anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kuhusu masheikh wa Taasisi ya Uamsho wanaoshikiliwa gerezani akidai utaratibu wa kisheria ufanyike ili waachiwe huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

error: Content is protected !!