Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Upatu, utakatishaji fedha wawapandisha kortini
Habari Mchanganyiko

Upatu, utakatishaji fedha wawapandisha kortini

Spread the love

MAGDALENA Uhwello na Halima Nsubuga leo tarehe 21 Agosti 2019, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka saba likiwemo ya utakatishaji fedha. Anaripoti Regina Mkonda … (endelea).

Mashitaka hayo yamesomwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Shitaka la kwanza; Wanatuhumiwa kula njama katika kusimamia na kuendesha shughuli za upatu, wakidaiwa kwamba walitekeleza kosa hilo katika tarehe tofauti mwaka 2017 wakiwa jijini Dar es Salaam.

Shitaka la pili; watuhumiwa hao wanadaiwa  kati ya tarehe 1 Aprili 2017 na Juni 30 2017, walisimamia shughuli za upatu kinyume cha sheria na kukusanya fedha kutoka kwa watu wakiwaahidi kupokea faida kutokana na fedha zao.

Katika shitaka la tatu; Watuhumiwa hao walisomewa kosa la utakatishaji fedha haramu wakidaiwa kwamba, kwenye nyakati tofauti mwaka 2017 wakiwa jijini Dar es Salaam, waliingiza Dola za Marekani 394,265 kwenye akaunti namba 3004211400319 kwa jina la Magdalena na Halima.

Fedha hizo ziliingizwa katika Benki ya Equity ya nchini Tanzania huku wakijua, pesa hizo ni mazalia ya kuendesha shughuli haramu za upatu kinyume cha sheria.

Shitaka la nne; Ni utakatishaji fedha wa kiasi cha Dola za Marekani 12,309 katika akaunti 1002100721913 ya Equity Benki ya Uganda yenye jina la Smart Protus Magara zilizotokana na shughuli za upatu.

Shitaka la tano; Ni utakatishaji fedha wa kiasi cha Dola za Marekani 29,086 wanazodaiwa kuziingiza katika akaunti 1002100721913 ya Equity Benki ya Uganda yenye jina la Smart Protus Magara.

Kwenye shitaka la sita; Watuhumiwa hao wanadaiwa kuficha chanzo cha fedha kiasi chaDola za Marekani 58,743 zilizoingizwa kwenye akaunti namba 1002100721913 ya Equity Benki ya Uganda yenye jina la Smart Protus Magara zilizotokana na shughuli hiyo.

Shitaka la saba; Ni utakatishaji fedha kiasi cha Dola za Marekani 83718 walizoingiza katika akaunti namba  1002100721913 ya Equity Benki Uganda yenye jina la Smart Protus Magara.

Washitakiwa wote wamekana mashtaka hayo. Baada ya kuwasomea mashtaka washitakiwa hao, Wakili Wankyo amesema, upelelezi wa shauri hiyo haujakamilika lakini uko katika hatua za mwisho na kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe kusikilizwa.

Hakimu Simba amewanyima dhamana washitakiwa kwa kuwa, mashtaka yao hayana dhamana. Hakimu Simba amepanga kesi hiyo ya jinai namba 167 ya mwaka 2019 kusikilizwa tarehe 30 Agosti 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!