BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imesimamiasha shughuli za Bodi ya Wakurugenzi na Uongozi wa Bank M. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
BoT imechukua hatua hiyo baada ya Benk M kushindwa kujiendesha kwa kukosa mtaji unaokubalika kisheria ambapo sasa BoT watasimamia uendeshaji wa benki hiyo.
Gavana wa BoT, Profesa Florens Luoga wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, amesema uamuzi huo umechukuliwa baada ya kubainika kwamba benki M ina upungufu mkubwa wa ukwasi kinyume na matakwa ya sheria ya kibenki.
Prof. Luoga amesema hatua hiyo imechukuliwa ili kulinda maslahi ya wateja na wakopeshaji wote wanaohusika na shughulia ambazo zilikuwa zikiendeshwa na Benki M.
“Kutokana na uamuzi huo, BoT imesimaisha bodi ya wakurugenzi na uongozi wa Banki M kuanzia leo, hivyo kutokana na uamuzi huo imemteua Meneja Msimamzi ambaye atakuwa na shughuli ya kusimamia benki hiyo kwa kipindi ambacho itakuwa chini ya usimamizi wa BoT,” amesema Prof. Luoga.
Katika nyingine, amesema shughuli za utoaji huduma za kibenki katika benki M zitasimama ndani ya siku 90 wakati BoT ikifanya tathimini ya hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa jambo hilo.
Sambamba na hilo, Prof. Luoga amesema wanahisa wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) na benki ya TPB wameamua kuunganisha benki hizo ili kuboresha ufanisi na utendaji wa benki hizo.
Prof. Luoga amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya BoT kuzipa muda wa miezi minne wa kuhakikisha zinafikisha kiwango cha mtaji kinachohitajika na sheria ya benki na taasisi za fedha, kitendo ambacho benki hizo kilishindwa kufikia n akuamua kuungana pamoja.
“Kufuatia muungano huo, kutakuwepo na benki moja ambayo itaendelea kuitwa benki ya “TPB Bank Plc”. Kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha 30(1)(a) cha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, Benki Kuu ya Tanzania imeridhia ombi la uunganishaji wa benki za TWB na TPB na kuwa benki moja kuanzia tarehe 03 Agosti 2018 itakayoendelea kuitwa benki ya “TPB Bank Plc” ambayo itaendelea kuwa na mtaji wa kutosha kama inavyotakiwa chini ya kifungu cha 17 cha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006,” amesema na kuongeza.
“ Hivyo, wateja, wafanyakazi, mali na madeni yote ya benki ya TWB yataunganishwa na yale ya benki ya TPB. Hivyo, muungano huu utaifanya benki mpya ya TPB Bank Plc kuwa imara zaidi na itakuwa ina mtaji wa kutosha kama inavyotakiwa kisheria chini ya kifungu cha 17 cha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006.
“Benki Kuu inawaomba wateja wa benki ya TWB kuwa watulivu katika kipindi cha mpito cha uunganishaji wa benki hizi na waendelee kupata huduma za kibenki kwa utaratibu utakaotolewa na menejimenti ya uongozi wa benki ya TPB.”
Leave a comment