UMOJA wa Mataifa (UN), ofisi za Tanzania umeitaka jamii kudumisha amani na kuhakikisha hapatokei migogoro ili kuenzi siku ya leo ambayo dunia inaadhimisha siku ya amani, anaandika Mwandishi Wetu.
Kauli hiyo imetolewa leo na Ofisa Habari wa UN, Stella Vuzo na kuongeza kuwa siku ya leo ni muhimu kwa jamii kwa kuwa inalenga kuelezea umuhimu wa kuwapo amani.
Amesema nchi nyingi duniani zinajaribu kuitafuta amani kwa muda mrefu japokuwa haijaipata na kwamba malengo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ni kuhakikisha kila mtu anaishi kwa amani.
Leave a comment