
Wanafunzi wa shule ya msingi
UKOSEFU wa Chakula sheleni hususan zile zinazomilikiwa na serikali umetajwa kuwa chanzo kikubwa kinasababisha wanafunzi kutoroka mashuleni na kwenda kujitafutia chakula hali inayoathiri taaluma na maendeleo ya elimu nchini. Anaandika Ferdinand Shayo, Arusha … (endelea)
Mwanakijiji wa kijiji cha Arkata, Kipara Ngine amesema kuwa watoto wengi wamekua wakitoroka shuleni kwa kukosa chakula hivyo kupelekea idadi ndogo ya mahudhurio mashuleni.
Kipara ameiasa saerikali kwa kushirikiana na mashirika binafsi pamoja na wazazi kuhakikisha upatikanaji wa chakula katika sahule ya msingi Arkata iliyopo wilaya ya Monduli mkoani hapa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Shule Kipi Alarosi amesema kuwa licha ya changamoto ya utoro bado shule hiyo inakabiliwa na uchakavu wa majengo na upungufu wa madarasa hivyo ameiomba jamii na wapenda maendeleo wajitokeze kuiwezesha shule hiyo iweze kufanya vizuri kitaaluma.
“Shule haina madirisha na majengo yamechakaa mvua ikinyesha inaingia mpaka darasani watoto hawasomi vizuri hata kipindi cha jua vumbi linajaa darasani “ Amesema Alarosi.
Mkurugenzi wa Shirika la wafugaji Monduli Pastoralist Development (MPDI), Erasto Sanare amesema kuwa baada ya kupokea ombi la shule hiyo watatua fedha za ukarabati wa madarasa ya shule hiyo ili kuwajengea watoto mazingira bora.
Amesema mwamko wa jamii ya wafugaji katika masomo umekua kwa kiasi kikubwa mashirika na watu binafsi yakijitoa kusaidia kutatua changamoto zao ili watoto wa wafugaji wapate elimu bora.
Shop Bán Clone Bán Token Tự Động Giá Rẻ – http://accs.vn