Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ukatili kijinsia wapingwa
Habari Mchanganyiko

Ukatili kijinsia wapingwa

Spread the love

MKURUGENZI Mtendaji wa kituo cha msaada wa kisheria cha Parallegal, Morogoro, Frola Masoi ameitaka jamii kuzingatia na kuzifuata sheria zilizopo kwenye katiba ya Tanzania zinazoitaka kuacha matendo ya ukatili wa kijinsia ili kukomesha vitendo hivyo, anaandika Christina Haule.

Masoi amesema, zipo sheria kwenye katiba ya Tanzania zinazosema binadamu wote ni sawa, kila mtu ana haki, sambamba na matamko na mikataba mbalimbali ikiwemo ya kimataifa ambayo imeridhiwa inayopinga masuala ya ukatili wa kijinsia ukiwemo mkataba wa kimataifa wa CEDAU, hivyo jamii haina budi kuzingatia.

“Licha ya Serikali ya Tanzania kutokuwa na sheria mahususi ya kupambana na ukatili wa kijinsia kwa ujumla ambayo hadi sasa watetezi wa masuala ya kijinsia wanaendelea kuipigania iwepo lakini zipo sheria hizo zinzopambana na masuala ya makosa ya kujamiiana ambazo pia kisheria zinasimama kutetea masuala ya ukatili wa kijinsia (GBV) kwa ujumla,” amesema.

Naye Ofisa Ufuatiliaji wa kituo  hicho, Augustino Ernest amesema mwaka 2016 walipokea kesi 246 kutoka kwa wakazi wa manispaa pekee huku tayari wameshapokea kesi 229 katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Mei mwaka huu 2017.

Amesema, ongezeko hilo limetokana na wasaidizi wa kisheria kutembea wilaya mbalimbali za mkoa wa Morogoro kuhamasisha jamii kupinga ukatili huo ikiwemo wilayani Kilosa kwa kutoa elimu na kufanya matukio hayo kuonekana kuongezeka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!