Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ujumbe wa Amnest kwa Rais Samia huu hapa
Kimataifa

Ujumbe wa Amnest kwa Rais Samia huu hapa

Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

 

SHIRIKA la Kimataifa la Kutetea Haki za Binaadamu (Amnesty International), limeshauri Serikali ya Tanzania kutumia kamati ya corona iliyoteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kushughulikia upatikanaji chanjo. Vyombo vya kimataifa vinaripoti … (endelea).

Katika taarifa hiyo iliyochapwa kwenye mtandano wa shirika hilo, Amnest imesifu hatua ya Rais Samia kutangaza tume ya kushughulikia virusi vya corona (COVID-19), na kwamba matumaini ya kupambana na corona yanaonekana.

Shirika hilo limeripoti kwamba, bado kuna kazi kubwa ya kukabiliana na virusi hivyo Tanzania, na kwamba ni wakati kwa tume hiyo kufanya utaratibu wa kupata chanzo kama ilivyo kwa mataifa mengine.

Taarifa hiyo imeeleza, Tanzania chini ya uongozi wa Hayati John Magufuli, kulikuwa na ukimya wa muda mrefu kuhusu mapambano dhidi ya virusi hivyo.

Amnesty limeeleza, iwapo chanjo hiyo itapatikana, Serikali ya Tanzania inapaswa kuhakikisha inaisambaza katika maeneo mbalimbali ya nchi, na kusiwe na ubaguzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!