Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Burudika Ujio wa Asa na ngoma mpya ‘Ocean’
Burudika

Ujio wa Asa na ngoma mpya ‘Ocean’

Spread the love

MWANAMUZIKI mahiri kutoka nchini Nigeria, Bukola Elemide maarufu kama ‘Asa’ ameachia ngoma yake mpya iitwayo Ocean aliyofanya na prodyuza maarufu, Prime, ikiwa ni maandalizi ya kutoa albamu yake ya V (Five) inayotarajiwa kuingia sokoni hivi karibuni. Anripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Kuachiwa kwa ngoma hiyo, kunakuja muda mfupi baada ya mwanadada huyo, kutoa ngoma nyingine, Mayana ambayo imepokelewa vyema na mashabiki wa muziki ndani na nje ya mipaka ya Nigeria.

 

Dairekta mkali, Meji Alabi ndiye aliyefanya video ya wimbo huo ambapo kwa kuzingatia mashairi na staili ya uimbaji ya Asa, ukichanganya na vionjo alivyoviweka dairekta huyo katika video hiyo iliyopo katika mfumo wa ‘visuals’, kwa pamoja vimeifanya video hiyo kuwa moto wa kuotea mbali.

Akiuzungumzia wimbo huo, Asa amenukuliwa akisema: “Ocean ni miongoni mwa kazi bora kabisa katika tasnia ya muziki. Nguvu za kujua mimi ni nani, nini nakitaka, kufanya ninachokitaka na kuishi maisha ya ukamilifu kama Mungu alivyoniumba.”

Ocean ni miongoni mwa ngoma zilizopo kwenye albamu ya V (Five) ya mwanadada huyo inayotarajiwa kuingia mitaani Februari 25 na ilitengenezwa dakika za mwisho kabla mwanadada huyo hajaamua kurudi Nigeria baada ya ziara za kimataifa za muziki, kuahirishwa kutokana na janga la Corona.

Pia mwanadada huyo anatarajia kufanya shoo jijini London, Uingereza Mei 3, 2022 katika Ukumbi wa Royal Albert Hall, ikiwa ni mwendelezo wa kuutangaza muziki wake kimataifa. Cheki video ya wimbo huo hapa: https://youtu.be/MIKNaODK4jk

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BurudikaMichezo

Kizz Daniel aunguruma na EP mpya ‘Thankz alot’

Spread the loveMKALI wa muziki nchini Nigeria, Kizz Daniel ametoa EP yake...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Burudika

Piga makofi kwa Mr. Eazi …achomoka na ‘The Evil Genius’

Spread the loveMAKOFI kwa Mr Eazi! Staa wa Afropop, Mr Eazi ameachia...

Burudika

Kishindo cha Afro B katika “Wo wo wo” akiwa na Rich the Kid&Rimzee

Spread the loveSTAA ambaye alitambulishwa na ngoma maarufu, Afrowave ‘Drogba’, Afro B,...

error: Content is protected !!