Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ujambazi wa Sabaya wahojiwa kesi ya Mbowe
Habari za SiasaTangulizi

Ujambazi wa Sabaya wahojiwa kesi ya Mbowe

Spread the love

 

PETER Kibatala, Wakili wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, amembana shahidi wa saba wa Jamhuri, Inspekta Mahita Omari Mahita, kuhusu matukio ya uhalifu yaliyokuwa yanafanywa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kibatala amembana Inspekta Mahita ambaye alikuwa Msaidizi wa Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Arusha, leo Ijumaa, tarehe 5 Novemba 2021, katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mawasiliano jijini Dar es Salaam, mbele ya Jaji Joackim Tiganga.

Wakili Kibatala alimbana Inspekta Mahita baada ya kutoa ushahidi wake mahakamani hapo, uliodai yeye na wenzake walipokea maelekezo kutoka kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Arusha (RCO), ACP Ramadhan Kingai ya kuzuia kundi linalodaiwa kuandaliwa na Mbowe, ili kufanya vitendo vya ugaidi.

Pia, kundi hilo linadaiwa kutaka kulipua vituo vya mafuta na kudhuru viongozi wa serikali akiwemo Sabaya.

Kwa sasa, Sabaya anatumikia kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya kukutwa na hatia ya unyang’anyi wa kutumia silaha pamoja na wenzake. Pia, kesi nyingine na wenzake sita ya kuendesha kundi la kihalifu inaendelea mahakamani Arusha.

Katika moja ya maswali aliyoulizwa na Kibatala ni suala la uhalifu uliokuwa ukifanywa na Sabaya wakati yeye Inspekta Mahita ambaye ni mtoto wa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) mstaafu Omar Mahita akiwa msaidizi wa mpelelezi.

Mahoajino ya Kibatala na shahidi huyo yalikuwa hivi;

Kibatala: Unafahamu kwamba Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya amehukumiwa na Mahakama kwa Makosa ya Ujambazi

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Kibatala: Je unafahamu kwamba Sabaya amehukumiwa makosa ya ujambazi wakati wewe ukiwa afisa wa polisi Arusha na ACP Kingai

Shahidi: Ndiyo natambua

Kibatala: Wewe ulifanya jukumu gani katika kuzuia uhalifu wa Sabaya

Shahidi: Siyo lazima mimi lakini kuna wasaidizi waliopo chini yangu walizipata

Kibatala: Na unafahamu kwamba matendo yake yalijirudia rudia

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Mwambie mheshimiwa Jaji iwapo wewe na afande Kingai kama mlipata taarifa za intelijensia kuhusu uhalifu wa Sabaya

Shahidi: Sikupata taarifa

Kibatala: Lakini unajua mipango ya uhalifu wa wilaya ya Hai, nje ya eneo lako la kazi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwanini tusiseme kwamba kesi hii nyinyi na Sabaya mlitengeneza kesi kwa ajili ya mambo ya Kisiasa

Shahidi: Siyo kweli kabisa

Kibatala: Huyu ASP Jumanne yupo wapi

Shahidi: Yupo Arumeru

Kibatala: Kwamba ufahamu kwamba Jumanne amesimamishwa kazi baada ya kumbambikia Mzee mstaafu kuwekewa meno ya tembo kwenye mzinga wake wa nyuki chini ya usimamizi wa ASP Jumanne ambaye ni shahidi wenu

Shahidi: Sifahamu najua yupo kazini

Kibatala: Muda huu tunapo ongea yupo ofisini?

Shahidi: Sifahamu kwa sababu siwasiliani naye siku nyingi

Kibatala: Na unajua tukio lake la kusimamia kumuwekea mzee wa watu meno ya tembo

Shahidi: Nafahamu

Kibatala: Je, ukimfahamisha huyu aliyetoka Kudhuliwa Sabaya

Shahidi: Sijamwambia

Kibatala: Ulimwambia mheshimiwa Jaji kwamba uliifahamisha kamati ya ulinzi ya wilaya Hai au Mkoa wa Kilimanjaro

Shahidi: Hapana Siku Mwambia

Kibatala: Katika briefing zenu, Je Kingai aliwambia kwamba ametoa taarifa kwa kati za ulinzi na usalama

Shahidi: Hakutuambia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!