HALI ya hewa nchini Uingereza inatarajiwa kuwa ya joto kali la kuvunja rekodi leo tarehe 19 Julai, 2022 na kufikia nyuzi 38 za joto.
Mamlaka ya hali ya hewa nchini humo imesema katika baadhi ya maeneo huenda joto likapindukia nyuzi 40 za joto. Inaripoti mitandao ya kimataifa… (endelea).
Baadhi ya shule zimeamua kufunga na watu wanaotumia treni kwa usafiri wameshauriwa kubaki nyumbani.
Aidha, maeneo ya kusini mwa Ulaya yameanza kupata ahueni baada ya wimbi la joto kali lililosababisha mamia ya vifo vya watu mwishoni mwa wiki iliyopita bado wazimamoto wanapambana na mioto ambayo inaendelea kuteketeza misitu.
Wanasayansi wametoa tahadhari, wakisema zaidi ya nusu ya eneo la Umoja wa Ulaya litakabiliwa na ukame.
Leave a comment