Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uhuru yafurika kumuaga Dk. Magufuli, vilio vyatawala
Habari za SiasaTangulizi

Uhuru yafurika kumuaga Dk. Magufuli, vilio vyatawala

Spread the love

 

MAELFU ya wakati wa mkoa wa Dar es Salaam na maeneo jirani, wamejitokeza kwa wingi kuuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, katika Uwanja wa Uhuru. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Leo Jumapili tarehe 21 Machi 2021, ni siku ya pili na ya mwisho kwa wakazi wa Dar es Salaam, kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Dk. Magufuli kisha kesho Jumatatu, utaagwa kitaifa mkoani Dodoma ambapo ni siku ya mapumziko.

Idadi ni kubwa ya wananchi katika Uwanja wa Uhuru ambao wamejitokeza hali inayowapa wakati mgumu vyombo vya ulinzi na usalama kuweza kuwaongoza.

Majukwaa yamejaa huku umati mkubwa ukiwa bado nje ukisubiri kuingia.

Idadi ya wale wanaoishiwa nguvu nayo ni kubwa na huku gari za wagonjwa zipo za kutosha ambazo zimekuwa zikitoka kuwapeleka hospitali mbalimbali kwa huduma zaidi.

Dk. Magufuli, alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena mkoani Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mfumo wa umeme.

Kutokana na idadi hiyo kuwa kubwa, Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene aliagiza polisi kusimamia vyema watu kuingia na kutoka ili watu wote waweze kutoa heshima za mwisho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!