Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Uhaba Maji: Aweso aagiza tenki kubwa kuwekwa Hospitali ya Muhimbili
HabariKitaifa

Uhaba Maji: Aweso aagiza tenki kubwa kuwekwa Hospitali ya Muhimbili

Spread the love

WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso ameagiza kuwekwa kwa tenki kubwa la maji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili kuhakikisha huduma ya maji inakuwa ya uhakika wakati wote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar…(endelea).

Aweso ametoa agizo hilo mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi Antony Sanga, leo Jumatatu tarehe 7 Novemba, 2022, walipotembelea hospitali hiyo kwa lengo la kuhakikisha huduma za maji zinaendelea kuwepo na kuweka mipango mizuri kwaajili ya baadae.

Aidha Waziri huyo ameagiza DAWASA ihakikishe inapeleka maji ya uhakika kwa sasa na kusaidia uwekaji wa maji ya akiba kama tahadhari kwa baadae.

Vilevile Aweso ameilekeza Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kutafiti haraka na kuchimba kisima ili kuwa na uhakika wa upatikanaji Maji.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohammad Janab amefafanua kuwa Hospitali inahitaji angalau akiba ya lita milioni sita.

Akitoa taarifa ya upatikanaji wa maji hospitalini hapo Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi ameeleza umuhimu wa kuwa na akiba ya maji ndani ya Hospitali zote nchini ili kuepusha usumbufu wowote kwa huduma za tiba kwa Wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!