Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Michezo Ugonjwa uliomuondoa Bi Hindu watajwa
Michezo

Ugonjwa uliomuondoa Bi Hindu watajwa

Chuma Selemani maarufu kama ‘Bi Hindu’
Spread the love

 

FAMILIA ya Muigizaji mkongwe nchini, Chuma Selemani maarufu kama ‘Bi Hindu’, imeweka wazi maradhi yaliyosababisha umauti wa mkongwe huyo kwenye sanaa ya uigizaji kuwa ni saratani ya mapafu. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Bi Hindu ambaye pia alikuwa mchambuzi wa masuala ya kijamii na kifamilia katika kituo cha Redio ya EFM ameripotiwa kufariki dunia leo tarehe 9 Julai 2022, asubuhi.

Kifo cha msanii huyo kimethibitishwa na mtoto wake Mwanaidi ambaye ameeleza kuwa Mama yake aliugua kwa muda mrefu na saratani iliyomshambulia mapafu.

Mwanaidi amesema kuwa Mama yake alikuwa akiuguzwa nyumbani “Mama tulikuwa tukimuuguza nyumbani ambapo alikuwa akisaidiwa kupumua kwa mashine ya Oxygen,” amesema.

Mwanaidi amesema kuwa Mama yake alikuwa mtu mashuhuri hivyo ni muhimu mashabiki zake na watanzania kwa ujumla wajue msiba huo ulipo na taratibu nyingine watazidi kutoa taarifa. Amesema msiba upo Magomeni mtaa wa Uweje.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!