Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Uganda kufungua shule Januari baada ya miaka miwili
Kimataifa

Uganda kufungua shule Januari baada ya miaka miwili

Yoweri Museveni
Spread the love

 

RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni ametangaza kuwa nchi hiyo itakuwa tayari kuanza shughuli za kawaida ifikapo Januari 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Uganda … (endelea).

Katika hotuba yake kwa taifa aliyoitoa juzi jana tarehe 29 Oktoba, 2021 amesema hatua ya hiyo imefikiwa baada ya kupatikana kwa chanjo za Covid-19.

Museveni amesema machifu na maofisa wengine wa serikali wanapaswa kuhakikisha kuwa wananchi wanapata chanjo katika maeneo yao.

Amesema kufikia Desemba 2021, nchi itakuwa imepata dozi milioni 23 za chanjo ya Covid-19.

“Hii itatosha kuwachanja watu milioni 12, ikiwa ni pamoja na makadirio ya wafanyakazi milioni 4.8 wa mstari wa mbele na watu walio hatarini, na kutuweka kwenye njia ya kufungua nchi kikamilifu,” amesema.

Pia amesema shule zitafunguliwa mwezi Januari mwakani bila kujali kama watu watakuwa wamechanjwa au lah, na kuongeza kuwa uamuzi utakuwa mikononi mwao.

“Niko hapa kuwaambia Waganda wote kwamba chanjo kwa wafanyakazi wote walio mstari wa mbele sasa zinapatikana. Tembea hadi kituo cha afya, ubebwe na bazukulu au nenda kwa baiskeli.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!