Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo UEFA yaitoa Man City kifungoni
Michezo

UEFA yaitoa Man City kifungoni

Spread the love

SHIRIKISHO la mpira wa miguu barani ulaya (UEFA) imeifungulia klabu ya Manchester city kutoka kwenye kifungo cha kutoshiriki michuano ya klabu bingwa barani humo kwa ngazi ya klabu kwa kipindi cha miaka miwili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… endelea

Timu hiyo ilifungiwa 14 februari, 2020 kwa kosa la kuvunja sheria za EUFA za leseni ya klabu na matumizi ya pesa na kupigwa faini Tsh. 74.9 Bilioni.

UEFA ilifungua uchunguzi huo baada ya kuwepo madai kuwa klabu hiyo imevunja vifungu kadhaa ya Sheria ya fedha iitwayo ‘Financial Fair Play – FFP’, lakini Klabu hiyo ilikana madai hayo na kusema haijavunja sheria yoyote

Sheria hiyo ilitengenezwa kuhakikisha kiasi cha fedha kinachotolewa na klabu katika kumnunua mchezaji na katika kumlipa vinakaribia kuwa sawa na kiasi mchezaji anachopata katika matangazo na fedha za tuzo

Mara baada ya kutoka adhabu hiyo, uongozi wa klabu hiyo uliamua kukata rufaa kwa mamlaka husika ndani ya shirikisho hilo na baada ya miezi mitano wakafanikiwa kushinda rufaa hiyo.

Timu ambayo kwa sasa inashika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu nchini England na hivyo itafaninikiwa kushiriki michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!