Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni
Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the love

BENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi ya Tawala za Mitaa (ALAT Taifa), ikiwemo kudhamini Mikutano yake Mikuu ya Mwaka kwa takribani miaka 7 mfululizo, na hadi sasa jumla ya Sh. 1.2 bilioni  zimeshatumika. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).


Makamu wa Rais wa Tanzania Dk. Philip Mpango akielezewa mafanikio na mipango iliyopo kati ya Benki ya NMB na ALAT Taifa katika ngazi zote, Afisa Mkuu Wateja Wakubwa na Serikali wa NMB, Alfred Shao, alipotembelea banda la NMB katika viwanja vya AICC Arusha, ulipokua unafanyika Mkutano Mkuu wa 37 wa ALAT Taifa.

Haya yamesemwa na Afisa Mkuu Wateja Wakubwa na Serikali wa NMB, Alfred Shao wakati akiwasilisha mada katika Mkutano wa 37 wa ALAT uliofanyika kwa siku tatu katika ukumbi wa AICC- Arusha ambapo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango alikuwa mgeni rasmi.

Afisa Mkuu Wateja Wakubwa na Serikali wa NMB, Alfred Shao, (kushoto) akimkabidhi Makamu Mwenyekiti wa ALAT Taifa, Sima Constantine Sima mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. Milioni 200 ikiwa ni udhamini wa NMB kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Jumuiya hiyo uliofanyika jijini Arusha. Akishuhudia ni Mkuu wa Idara ya Biashara za Serikali Benki wa NMB – Vicky Bishubo.

 Mkutano huo uliokuwa na kauli mbiu inayosema “Miundombinu iliyoboreshwa ni chachu ya utoaji wa huduma bora katika Mamlaka za Serikali za Mitaa” uliwakutanisha zaidi ya watumishi 500 kutoka Halmashauri zote 184 za Majiji, Manispaa, Wilaya na Miji kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Aidha, Shao alielezea kuwa, Benki ya NMB kama mdau wa maendeleo kupitia Halmashauri zote chini, imekuwa mshirika mkubwa kuboresha miundombinu ya elimu, afya, usafirishaji na mazingira.

Afisa Mkuu Wateja Wakubwa na Serikali wa NMB , Alfred Shao, akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango, kwa niaba ya Benki ya NMB kwa kudhamini Mkutano Mkuu wa 37 wa ALAT Taifa kwa Sh. 200 milioni. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angella Kairuki pamoja na Makamu Mwenyekiti wa ALAT Taifa. Constantine Sima (katikati).

Alisema pia NMB inaendelea kushiriki kikamilifu katika kutoa dhamana kwa kandarasi zaidi ya 580 zenye thamani ya Sh 49 bilioni katika hatua zote kuanzia hatua ya kuomba na kutekeleza miundombinu chini ya TARURA.

Alisema kupitia mifumo na mtandao mpana wa NMB umesaidia Serikali katika makusanyo ya mapato ya zaidi ya Sh. 9.8 trilioni kuanzia mwaka 2018.

“Lakini pia, kwenye utunzaji wa mazingira tumezindua kampeni ya upandaji miti milioni moja nchi nzima, ambapo hadi sasa tumepanda miti zaidi ya 550,000.

“NMB imetenga kiasi cha Sh 472 milioni kama zawadi katika kampeni ya Tunza Mti Tukutuze kwa shule za Halmashauri zote Bara na Visiwani kushirikiana na Wizara ya TAMISEMI,” amesema.

Akisisitiza umuhimu wa kuyatunza mazingira kwa ajili ya maendeleo endelevu, Dkt. Mpango alizihamasisha Halmashauri kushiriki kikamilifu na kuwataka kufanya kama NMB walivyofanya kwenye kampeni ya kupanda miti milioni moja ambapo kwa kushirikiana na TAMISEMI wameandaa shindano la shule la upandaji miti lenye zawadi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!