Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Uchaguzi wa Simba wapigwa Stop
Michezo

Uchaguzi wa Simba wapigwa Stop

Spread the love

KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) chini ya Mwenyekiti wake, Wakili Revocatus Kuuli imetangaza kuusimamisha Uchaguzi Mkuu wa klabu ya Simba kutokana na kuwepo kwa dosari mbalimbali za kikanuni za wanachama wa TFF. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Dosari ambazo zimejitokeza katika uchaguzi huo wa Simba ni pamoja na kutowekwa kwa matakwa ya kisheria kama kuhusisha Kamati ya Rufaa na Kamati ya Maadili huku sheria ikiwataka kutumia kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF.

“Ni kweli tumesimamisha mchakato huo ili wafanye maboresho, zipo dosari tumeziona kama kamati na kama wakizifanyia kazi wataendelea na uchaguzi,” amesema Kuuli.

Aidha aliongezea ya kuwa kanuni za wanachama zinataka mgombea wa nasafi ya mwenyekiti achukue fomu kwa Sh. 200,000 na nasafi nyingine ni Sh. 100,000 lakini kamati ya Simba wao wameamua kuweka kiwango cha Sh. 500,000 kwa madai kwamba wanatumia kanuni cha uchaguzi za TFF.

Uchaguzi huo ambao wagombea katika nafasi tofauti tofauti walisharudisha fomu na kuingia katika hatua ya usahiri, huku uchaguzi huo hapo awali ulipangwa kufanyika Novemba 3 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!