Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 24 – Serikali
Habari za SiasaTangulizi

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 24 – Serikali

Spread the love

KITENDAWILI kuhusu tarehe rasmi ya kufanyika kwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini, sasa kimeteguliwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Seleman Jafo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), ametangaza kuwa tarehe 24 Novemba 2019 ndio siku ya kufanya uchaguzi huo leo tarehe 23 Agosti 2019 jijini Dodoma.

 “Kwa mujibu wa kanuni za uchgauzi wa serikali za mitaa mwaka 2019 ibara ya 4 ibara ndogo ya 1 na 3, waziri mwenye dhamana ya tawala za mitaa na serikali za mitaa anawatangazia umma na vyama vyote vya siasa vyenye usajili wa kudumu kuwa, uchaguzi ni tarehe 24 Novemba 2019,” amesema Jaffo.

Akielezea sehemu ya ratiba ya zoezi hilo, Jaffo amesema upigaji kura utaanza majira ya saa 2.00 asubuhi na kumalizika saa 10 Alasiri.

Amesema, wasimamizi wa uchaguzi watatoa maelekezo ya uchaguzi huo siku 62 kabla ya siku ya uchaguzi, wakati watumishi watakaosimamia zoezi la uandikishaji na uandaaji orodha ya wapiga kura  watateuliwa siku 52 kabla ya uchaguzi.

Pia, amesema uandikishaji na uandaaji orodha ya wapiga kura utaanza siku 47 kabla ya uchaguzi siku ya uchaguzi huo ambapo zoezi hilo litafanyika ndani ya siku saba. Fomu za uteuzi zitachukuliwa siku 26 kabla ya siku ya uchaguzi na wahusika watarejesha fomu hizo ndani ya siku saba tangu siku ya kwanza ya kuchukua.

“Ukomo wa madaraka katika nafasi zote zilizogombewa mwaka 2014, viongozi hao watakoma kushika nafasi ya uongozi siku saba kabal ya siku ya wagombea kuchukua fomu ya uteuzi,” amesema Jaffo.

Jaffo amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uandikishaji na upigaji kura kwa ajili ya kuchagua viongozi bora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!