Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi Serikali za Mitaa: TLP, UMD, DP kuanza kampeni kesho
Habari za Siasa

Uchaguzi Serikali za Mitaa: TLP, UMD, DP kuanza kampeni kesho

Spread the love

VYAMA visivyokuwa na uwakilishi bungeni, TLP, UMD na DP, kesho tarehe 17 Novemba 2019  vitaanza kufanya kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Hayo wamesema viongozi wa vyama hivyo, katika nyakati tofauti leo tarehe 16 Novemba, 2019, wakati wakizungumza na mtandao wa MwanaHALISI ONLINE, kwa njia ya simu.

Augustino Mrema, Mwenyekiti wa Chama cha TLP, amesema atazindua kampeni za chama hicho, katika Kijiji cha Kiraracha, Marangu Magharibi, mkoani Kilimanjaro.

“Mimi kesho nitazindua kampeni za chama changu kwenye kijiji changu cha Kiraracha, Marangu Magharibi, jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro,” amesema Mrema.

Abdul Mluya, Katibu Mkuu wa chama cha DP, amesema chama chake kitazindua kampeni za uchaguzi huo, katika wilayani Buhingwe, mkoani Kigoma.

Hata hivyo, Mluya amedai kuwa, wagombea wake wengi wanashawishiwa na baadhi ya wananchi kujitoa katika uchaguzi huo.

Kamana Mrenda, Mwenyekiti wa Chama cha UMD, ameeleza kuwa, wamejipanga vyema kufanya kampeni katika maeneo waliyosimamisha wagombea. Na kwamba, chama chake kitazindua katika wilayani Kabondo mkoani Kigoma.

Kampeni za uchaguzi huo zinatarajia kuanza kesho, na kumalizika tarehe 23 Novemba mwaka huu. Kisha uchaguzi utafanyika tarehe 24 Nove,ba 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!