Saturday , 9 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi Mkuu 2020: Takukuru yamtia mbaroni Aden Rage
Habari za SiasaTangulizi

Uchaguzi Mkuu 2020: Takukuru yamtia mbaroni Aden Rage

Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Tabora nchini Tanzania, inamshikilia Ismail Aden Rage kwa tuhuma za rushwa na kuanza kampeni kabla ya wakati za uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora … (endelea).

Rage alishikiliwa na Takukuru kuanzia tarehe 23 hadi 24 Mei, 2020 alipoachiwa kwa dhamana baada ya taasisi hiyo, kupokea taarifa kuwa Mkurugenzi huyo wa Voice of Tabora FM aliwakusanya viongozi wa kata na matawi wa CCM kwa lengo la kuwashawishi wampigie kura.

Taarifa ya Mussa Chaulo, Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Tabora aliyoitoa leo Jumatatu tarehe 25 Mei, 2020 imesema uchunguzi wa suala hilo unaendelea.

Chaulo amewaonya wale wote walioanza kujipitisha ili kufanya ushawishi kwa wanachama ili wawachagua watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Rage aliwahi kuwa mbunge wa Tabora Mjini kupitia CCM kati ya mwaka 2010 na 2015.

Pia, amewahi kuwa Rais wa klabu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataka jamii inayohoji mafisadi

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan ametoa maagizo juu ya uboreshaji dira...

Habari za SiasaTangulizi

Kapinga: Kukatika kwa umeme siyo hujuma

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali ipo kazini...

error: Content is protected !!