Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Tangulizi Uchaguzi Marekani: Trump kukimbilia mahakamani
Tangulizi

Uchaguzi Marekani: Trump kukimbilia mahakamani

Spread the love

DONALD Trump, Rais wa Marekani amesema, uchaguzi mkuu nchini humo uliofanyika jana Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 umekubwa na udanganyifu na kupanga kwenda Mahakama ya Juu nchini humo.

Rais Trump anayetetea nafasi hiyo kupitia Chama cha Republican, anachuana vikali na mgombea wa Demokratic, Joe Biden.

Akizungumza na wafuasi wake mapema leo Jumatano wakati shughuli ya kuhesabu kura ikiendelea, Trump amesema ameshinda uchaguzi huo ingawa bado mamilioni ya kura zilizopigwa hazijahesabiwa.

“Ukweli ni kwamba tumeshinda, uchaguzi umekubwa na udanganyifu” amesema Trump huku akisisitiza kwamba sheria lazima zifuatwe na “tutakwenda Mahakama ya Juu, kama upigaji kura utaendelea.”

Uamuzi huo wa Trump kutaka kwenda mahakamani kupinga matokeo hayo, kutamaanisha mshindi akachelewa kupatikana.

Rais Trump amesema kinachotokea ni aibu “kwa nchi yetu.”

Mchuano bado ni mkali ambapo Biden anaongoza dhidi ya Trump katika majimbo yaliyokwisha kuhesabiwa kura zake na mchuano umejikita zaidi katika majimbo ya, Wisconsin, Pennsylvania, Arizona, Georgia na Michigan.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali kuhusu matokeo ya uchaguzi huo

2 Comments

  • Halafu eti wanataka kutufundisha Waafrika maana ya demokrasia. Huko kwao chaguzi zao zimejaa vurugu na tuhuma kibao. Wanasau boriti jichoni mwao. Huo ni ubeberu

  • Huko ndo kuna demokrasia ukiwa na wasi wasi unaenda mahakani kupata haki yakk sio huku bongo lala kwa huyu dikteta uchwara kwa wezi wasio na aibu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

Habari za SiasaTangulizi

Mawakili wa Chadema wabadilishia gia angani

Spread the loveMAWAKILI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameiomba Mahakama...

Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Jesca Kishoa avunja ndoa na Kafulila

Spread the love  NDOA baina ya Jesca David Kishoa, mbunge wa Viti...

error: Content is protected !!