Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi Buhigwe, Muhambwe: ACT-Wazalendo yakubali kushindwa
Habari za SiasaTangulizi

Uchaguzi Buhigwe, Muhambwe: ACT-Wazalendo yakubali kushindwa

Spread the love

 

LICHA ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kutotangaza matokeo rasmi ya chaguzi mdogo wa Ubunge wa Buhigwe na Muhambwe, mkoani Kigoma, Chama cha ACT-Wazalendo, kimekipongeza Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kutwaa majimbo hayo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Katika uchaguzi huo uliofanyika leo Jumapili tarehe 16 Mei 2021, ACT-Wazalendo kilichuana vikali na CCM, ambapo wagombea wao walikuwa; Jimbo la Muhambwe Dk. Florence Samizi (CCM) na Julius Masabo (ACT-Wazalendo) na Buhigwe waliogombea, Galula Kudra (ACT-Wazalendo) na Mwalimu Eliadory Kavejuru (CCM) .

Baada ya uchaguzi huo kumalizika, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amekipongeza CCM kwa kushinda katika Jimbo la Muhambwe, huku akiwapongeza wasimamizi wa uchaguzi huo.

 

“Nawapongeza CCM kwa ushindi wa halali kabisa Jimbo la Muhambwe. Kila la Kheri kwa Mbunge mpya. Tutakutana Uchaguzi unaofuata tukiwa Imara zaidi.”

“Nampongeza Msimamizi wa Uchaguzi wa Muhambwe na OCD wa Kibondo kwa kufanya kazi kwa weledi. Ninalaani matukio ya kuumiza watu yaliyotokea,” ameandika Zitto katika ukurasa wake wa Twitter.

Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo amesema, kwa mujibu wa matokeo yaliyokusanywa na mawakala wa chama hicho, mgombea wao katika Jimbo la Muhambwe amepata asilimia 41 ya kura.

“Tumekusanya matokeo ya uchaguzi katika vituo vyote 336 vya kupigia kura Jimbo la Muhambwe. Kura zetu, 41% ya kura zote, haziwezi kutupa Ushindi. Uchaguzi uliendeshwa vizuri. Kasoro kadhaa zilizojitokeza zisingebadili matokeo. Tunatumia uchaguzi huu kama Mafunzo kujiimarisha zaidi,” ameandika Zitto.

Naye aliyekuwa mgombea wa ACT-Wazalendo Muhambwe, Masabo kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika “A Fairly Win to the CCM (ushindi halali kwa CCM) Uhambweni.”

Kuhusu uchaguzi wa Muhambwe, Zitto amedai mchakato wake ulikuwa na dosari, hivyo chama chake kimepata funzo.

“Kwa upande wa Jimbo la Buhigwe, uchaguzi ulivurugwa. Matendo yale yale yaliyofanywa katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 Ndio yamefanywa Mwaka huu Buhigwe. Tuna mafunzo tumepata katika kuendelea kujenga chama chetu Kwa ajili ya chaguzi zijazo,” ameandika Zitto.

Hata hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Shaka Hamdu Shaka, amesema chaguzi hizo hazikuwa na dosari zozote, bali ACT-Wazalendo kimeshindwa kutokana na kushindwa kujiandaa vyema na kushiriki chaguzi hizo.

“Chama chake kimeshindwa kuingiza timu uwanjani iliyojiandaa vizuri, sisi tumejiandaa muda mrefu na wagombea wetu wanakubalika bila shaka yoyote” amesema Shaka.

Chaguzi hizo ndogo zimeitishwa na NEC, baada ya aliyekuwa Mbunge wa Muhambwe, Atashatsta Nditiye, kufariki dunia, na aliyekuwa Mbunge wa Buhigwe, Dk. Philip Mpango, kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!