Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Uamuzi kesi ya kina Mdee leo
Habari MchanganyikoTangulizi

Uamuzi kesi ya kina Mdee leo

Spread the love

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu ya Dar es Salaam, inatarajia kutoa uamuzi dhidi ya maombi yaliyofunguliwa na wabunge viti maalum 19, wakiongozwa na Halima Mdee, ya kuomba kibali cha kufungua kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama wa chama cha Chadema. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa leo Ijumaa, tarehe Julai 202, mahakamani hapo mbele ya Jaji Mustafa Ismail.

Mahakama hiyo inatarajiwa kutoa uamuzi kama inatoa kibali cha kufunguliwa kesi hiyo  ya kina Mdee kupinga kuvuliwa uanachama wa Chadema, au la.

Uamuzi huo ulikuwa utolewe juzi Jumatano tarehe 6 Julai, 2022, lakini ilishindikana baada ya mahakama kusema bado haujakamilika.

Mdee na wenzake wanadai, mchakato wa kuwafukuza uanachama ulikuwa kinyume cha Katiba ya Chadema na Katiba ya nchi.

Miongoni mwa hoja hizo Tano ni, maombi ya kuomba mapitio hayo yalifunguliwa ndani ya muda kisheria, wabunge hao kuwa na maslahi dhidi ya mchakato huo wakidai uliwaathiri kufuatia hatua ya Chadema kuwavua uanachama.

Nyingine ni, mchakato huo kuingiliwa na upendeleo kufuatia ya wajumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, waliowafukuza uanachama, kushiriki kikao Cha Baraza Kuu la Chadema, kilichotupilia mbali rufaa zao za kupinga kufukuzwa.

Hoja nyingine ni maamuzi ya Chadema kuwafukuza uanachama kuwa ya umma na mwisho ikiwa wabunge hao kukosa nafasi ya kupata haki Yao ya kusikilizwa juu ya uamuzi huo.

Mbali na Chadema iliyoshtakiwa kupitia Bodi yake ya Wadhamini, wajibu maombi wengine katika shauri hilo ni, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Mwansheria Mkuu wa Serikali (AG).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!