Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uamuzi kesi kina Mbowe leo, maombi yatawala
Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi kesi kina Mbowe leo, maombi yatawala

Spread the love

 

KESI ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu, inaendelea leo Jumanne, tarehe 14 Desemba 2021, kwa Mahakama Kuu, Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, jijini Dar es Salaam kutoa uamuzi wa kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Uamuzi huo, unahusu pingamizi la upande wa utetezi waliloweka dhidi ya maelezo ya onyo ya mshtakiwa Mohamed Ling’wenya yasipokelewe mahakamani kama kilelezo wakidai, hakuwahi kuyatoa bali alilazimishwa kuyasaini, baada ya kuteswa alipokamatwa.

Jaji Joachim Tiganga anayesikiliza kesi hiyo, ndiye atakayetoa uamuzi huo na tayari washtakiwa wote wanne akiwemo Mbowe wamefikishwa mahakamani hapo na Jeshi la Magereza.

Kama kawaida, Mbowe na wenzao wameonekana wakiwa na nyuso za tabasamu wakati wakiwasili mahakamani hapo, Mawasiliano jijini Dar es Salaam na kupokewa na wanachama na viongozi wa Chadema.

Maombi mbalimbali yalitawala eneo hilo kwa kila mmoja kuwaombea washtakiwa hao huku wengine wakiwa wameshikilia bibilia na wengine wamepiga magoti.

Mbali na Mbowe na Ling’wenya, washtakiwa wengine ni Adam Kasekwa na Halfani Bwire.

Kasekwa, Ling’wenya na Bwire waliowahi kuwa makomandoo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kikosi 92KJ, mkoani Morogoro.

Washtakiwa wote wanne, wanatuhumiwa kwa makosa ya kupanga vitendo vya kigaidi maeneo mbalimbali nchini Tanzania ikiwemo Kilimanjaro, Dodoma, Dar es Salaam na Arusha kwa kulipua vituo vya mafuta, kufanya vurugu kwenye mikusanyiko ya watu na kudhuru viongozi wa umma.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!