Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Twitter na Facebook, zamfungia Trump
Kimataifa

Twitter na Facebook, zamfungia Trump

Rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump
Spread the love
MITANDAO ya Twitter na Facebook, imezifunga kwa muda akaunti za rais wa Marekani, Donald Trump, kufuatia kutuma ujumbe kwa wafuasi wake waliovamia Bunge. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Katika ujumbe uliotumwa katika mitadao hiyo kwa waandamanaji hao, Rais Trump alisema, “nawapenda” na kuwataka kwenda nyumbani.

Twitter na Facebook wameeleza pia kuwa Rais Trump ametoa madai ya uongo kuhusu udanganyifu uliofayika katika uchaguzi huo.

Twitter ilisema, Rais Trump anapaswa kuondoa jumbe zake tatu alizoweka kutokana na ukiukwaji wa maadili.

Kampuni hiyo imesema, iwapo Trump atakaidi agizo la kufuta jumbe zake hizo, akaunti zake za twitter zitafungwa kabisa.

Imesema, “ukiukaji wa sheria za twitter siku zijazo utasababisha kufutiliwa mbali kwa akaunti ya @realDonaldTrump account.”

https://twitter.com/TwitterSafety/status/1346970432017031178

Hatua hiyo ina maana kwamba siku za Donald Trump katika mtandao wa twitter zinahesabika.

Rais huyo anajulikana kwa kutoheshimu masharti ya muongozo wa twitter kuhusu jamii.

Nayo kampuni ya facebook imemfunga Rais Trump kwa saa 24, na kwamba YouTube pia iliondoa video hiyo.

Facebook imesema: Tuliiondoa kwasababu tuliamini kwamba inachochea badala ya kupunguza ghasia zilizokuwa zikiendelea.

Wafuasi wake walivamia Bunge la Marekani na kukabiliana na maafisa wa polisi kitu kilichosababisha kifo cha mwanamke mmoja.

Ghasia hizo zilisitisha mjadala kuhusu ushindi wa rais mteule, Joe Biden.

Kabla ya ghasia hizo, rais Trump aliwaambia wafuasi wake mjini Washington kwamba uchaguzi huo uliibwa.

Saa chache baada ya ghasia kuzuka ndani na nje ya jumba la Capitol Hill, alionekana katika video akirejelea madai hayo ya uongo.

You tube ilisema kwamba iliiondoa kanda hiyo ya video kwasababu ilikiuka sera za kusambaza madai ya udanganyifu kuhusu uchaguzi uliopita.

Awali twitter haikuwa imeiondoa video hiyo, na badala yake kuondoa uwezo wake wa kujibiwa, kupendwa na kutolewa maoni.

Lakini baadaye iliiondoa na kufuta akunti ya rais huyo anayeondoka madarakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!