TIMU ya soka ya wanawake ya Tanzania ‘Twiga Stars’ imetinga fainali ya michuano ya COSAFA inayofanyika nchini Afrika Kusini. Anaripoti Damas Ndelema, TUDARCo … (endelea).
Ni baada ya kuwaondoa Zambia kwa mikwaju ya penati 3-2, leo Alhamisi, tarehe 7 Oktoba 2021.
Twiga na Zambia zilifika hatua ya kupigiana penati, baada ya kwenda sare ya 1-1 dakika 90.
Twiga walikuwa kwanza kupata bao dakika ya 17 kipindi cha kwanza kwa Zambia kujifunga. Zambia walirudisha goli hilo dakika ya 69 kupitia kwa mshambuliaji wao Chanda.
Katika mikwaju ya penati, mlinda mlango wa Twiga, Janeth Simba alipangua miwili kati ya tano zilizopigwa na kuwaondoa Zambia.
Nahodha wa Twiga, Amina Bilal amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.
Aidha, ikumbukwe tangu mashindano haya yaanze, Twiga wameruhusu bao moja katika mechi nne na hawajapoteza mchezo wowote ule katika michuano hiyo.
Hivyo, Twiga itasubiri mshindi kati ya wenyeji Afrika Kusini na Malawi watakaoumana katika fainali ya michuano hiyo ya COSAFA.
Leave a comment