Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu kurejea nchini muda si mrefu
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu kurejea nchini muda si mrefu

Samia Suluhu, Makamu wa Rais akimsalimia Tundu Lissu alipokuwa hospitali Nairobi
Spread the love

 

ALIYEKUWA mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, ametaka kuhakikishiwa usalama wake na serikali, ili aweze kurejea nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lissu ambaye ni makamu mwenyekiti wa chama cha Chadema (Bara) amesema, ataweza kurejea nchini mara moja, ikiwa atapa hakikisho la usalama wake kutoka kwa serikali.

“Nilisharejea nchini Agosti mwaka jana. Lakini nikalazimika kuondoka, baada ya kuwapo tishio jipya la usalama wangu,” ameeleza mwanasiasa huyo ambaye kwa sasa yuko nchini Ubelgiji.

Lissu alikwenda Ubelgiji kwa mara ya kwanza Januari 2018, baada ya kushambuliwa na kwa risasi na wanaoitwa na serikali, “watu wasiojulikana,” nyumbani kwake, Area D, mjini Dodoma.

Mara baada ya shambulio hilo, lililofanyika tarehe 7 Septemba 2017, Lissu alisafirishwa kwa ndege hadi katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya ambako alipokea matibabu kabla ya kuhamishiwa Ubelgiji kwa matibabu maalumu.

Alirejea tena nchini humo, muda mfupi baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani wa 28 Oktoba mwaka jana.

Amesema, anahofia sana uamuzi wa kumuondolea walinzi wa usalama wake ambao alipewa mwaka 2020 alipogombea kiti cha urais, kwani uamuzi huo unatishia maisha yake.

“Baadaye nilikamatwa na kuachiliwa, kabla ya kukamilisha mchakato ambao uliniwezesha kutoroka nchi. Kwahiyo, ningependa kuwa na hakikisho katika suala hili kwa sababu Rais Samia Suluhu Hassan anafahamu hili vyema baada ya kunitembelea katika Nairobi Hospital,” alisema.

Akaongeza, “ninataka kujua watu waliojaribu kuniua, na usalama wangu nitakaporudi nyumbani. Je, hizo kesi za…zitaendelea na ikiwa nitaruhusiwa kushiriki katika siasa.”

Kwa mujibu wa maelezo yake, Lissu alifanikiwa kuondoka nchini, baada ya nchi wahisani kuingilia kati kwa kuiomba serikali ya Rais John Magufuli, kumruhusu kuondoka.

Mengine ambayo mbunge huyo wa zamani wa Singida Mashariki, ameeleza kuwa anapenda yafanyike, ni kurejeshewa gari lake, ambalo alikuwa amelitumia siku aliyonusurika na risasi 16, mjini Dodoma.

Aidha, Lissu ametaka hakikisho la serikali kuwa itamlipa gharama za matibabu aliyotumia, mafao yake kama mbunge wa zamani na kuangaliwa upya kwa kesi zilizofunguliwa dhidi yake.

Tundu Lissu alipokuwa anasafirishwa kupoka Dodoma kwenda Nairobi

Kauli ya Lissu inakuja, wakati Rais wa Tanzania, Samia Suluhu, akiahidi kukutana kwa mazungumzo na viongozi wa upinzani.

Amesema, angependa kujua hatma ya mafao yake kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2015 hadi 2019 wakati alipofahamishwa kuhusu kutostahili kwake kuwa mbunge wa Singida Mashariki.

Akiongea kwa hisia kali, Lissu alisema, “sijapokea malipo ya gharama za matibabu (kutoka kwa serikali). Hili Rais Hassan ambaye alinitembelea katika hospitali ya Nairobi Hospital analifahamu. Ninahitaji kujua ni kwanini sijalipwa.”

Rais Samia Suluhu, alipokuwa Makamu wa Rais akimsalimia Tundu Lissu alipokwenda  hospitali Nairobi kumjulia hali

Msemaji wa jeshi la polisi nchini Tanzania, David Misime amesema, uchunguzi juu kesi ya Lissu ulisimamishwa baada ya kukataa kujibu ombi la polisi la ushirikiano katika uchunguzi huo.

Akaongeza, “hawezi kukamatwa … lakini anapaswa kuripoti na kutoa maelezo.”

Amesema, polisi wana wajibu wa kisheria wa kuwalinda watu na mali zao bila kujali utaifa wao, kutambua, kuzuia na kutekeleza sheria ili kuimarisha amani, na usalama.
Kuna uwezekano mkubwa Lissu akarejea nchini, kufuatia hatua ya Rais Samia kutaka maridhiano na vyama vya upinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!