Friday , 2 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Tumieni fursa zinazojitokeza-Mavunde
Habari Mchanganyiko

Tumieni fursa zinazojitokeza-Mavunde

Spread the love

ANTONY Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Rais anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, amewataka vijana kutumia vyema fursa wanazozipata ili kujiingizia kipato badala ya kukaa vijiweni. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Mbali na hilo amesema, umefika wakati wa kuondokana na dhana ya kusubiri ajira kutoka serikalili, badala yake watumie fursa mbalimbali zinazojitokeza.

Mavunde ametoa kauli hiyo leo tarehe 24 Septemba 2019, wakati wa kukabidhiwa pikipiki 30 za usambazaji bidhaa zenye thamani ya zaidi ya Sh. 108 Mil kutoka Kampuni ya RoutePro na kuzikabidhi kwa vijana 30 kutoka mikoa mitano.

Amesema, serikali inatambua kuwepo kwa changamogo ya ajira kwa vijana.

“Ukosefu wa ajira kwa vijana ni moja ya changamoto inayolikabili taifa letu, ili kukabiliana nalo serikali imekuwa ikitoa kipaumbele kushirikiana na wadau wanaoonesha nia ya kusaidia kubuni mipango endelevu ya kuwezesha ajira kwa vijana.

“Kama ilivyofanya Kampuni ya Route Pro, kwa kutoa mafunzo ya biashara kwa vijana wetu. Tutaendelea kutoa ushirikiano  mkubwa kufanikisha suala hili la ajira linatatuliwa,” amesema Mavunde.

Jaja Mbazila, Meneja Uratibu wa Kampuni ya Route Pro akizungumza katika zoezi hilo amesema, kampuni hiyo imepata walengwa wa kushirikiana nao katika mpango huu.

Na kwamba, ni kutokana na rekodi  ya vijana ambao imewahi kufanya nao kazi katika miradi  mbalimbali ya usambazaji bidhaa katika siku za nyuma.

“Tumelenga kuwawezesha vijana wenye bidii ya kazi na kujituma kupata fursa kuwa na biashara zao, tumefanya nao kazi kwa karibu katika miaka iliyopita na wameonesha kuwa na nia ya kufanya vizuri biashara ya usambazaji,” amesema Mbazila na kuongeza;

“Mbali na kuwapatia pikipiki, RoutePro itawapatia vijana hao kiasi cha shilingi 100,000 kila mmoja ziwasaidie kuanzia kazi.”

Amesema, baada ya miezi 24 pikipiki hizo zitakuwa mali yao kwa ajili ya kuwasaidia katika shughuli za usambazaji “ingawa watakaopenda kufanya kazi katika mpango huu wa Route Pro wa kuwezesha vijana watajiunga tena katika mpango wa miaka 2 na kupatiwa tena tena pikipiki mpya.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

Habari Mchanganyiko

Dk. Gwajima atoa maelekezo kwa maofisa maendeleo nchini

Spread the love  WAZIRI wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto,...

error: Content is protected !!