JESI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeeleza kufanikiwa kuzima tukio la ujambazi, Mbezi Msakuzi, njia panda ya Mpiji Magoe. Anaripoti Kamote…(endelea).
Limeeleza, mafanikio hayo yametokana na taarifa kutoka kwa raia wema kwamba, kulikuwepo mpango wa kuvamia Saccoss ya Msakuzi tarehe 26 Septemba 2019.
Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 10 Oktoba 2019 na Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam wakati akizungumza na wanahabari.
“Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu Dar es Salaam kupitia kikosi kazi kilichokuwa kimeweka mtego, na ilipofika majira ya saa sita mchana zilifika pikipiki mbili aina ya boxer ambazo hazikusomeka namba zikiwa na majambazi wane.
“Mmoja kati yao akiwa na bastola, ndipo walipoona polisi na kuanza kukimbia huku wakirushiana risasi, lakini askali mahiri walipofanikiwa kuwajeruhi wawili,” amesema.
Amesema, majeruhi hao walipopekulia, walikutwa na bastola moja, risasi tatu ndani ya magazine na maganda mawili ya risasi ambapo walipelekwa hospitali na baadaye kufariki.
“Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu, kupitia kikosi kazi chake kimefanikiwa pia kumuua jambazi hatari aliyekuwa anatafutwa kwa muda mrefu kwa kufanya matukio mbalimbali ya mauaji na ujambazi.
“Tarehe 30 Septemba 2019 saa saba mchana, Jeshi la Polisi lilipta taarifa kutoka kwa msiri wake kuwa, Ilala Boma kuna jambazi sugu anayefahamika ka jina la Emmanuel Peter maarufu kwa jina la Mark Silengo na wenzake wanne, wanapanga mipango ya kwenda kufanya uhalifu,’ amesema.
Leave a comment