Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tumezima tukio la ujambazi -Kamanda Mambosasa
Habari Mchanganyiko

Tumezima tukio la ujambazi -Kamanda Mambosasa

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

JESI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeeleza kufanikiwa kuzima tukio la ujambazi, Mbezi Msakuzi, njia panda ya Mpiji Magoe. Anaripoti Kamote…(endelea).

Limeeleza, mafanikio hayo yametokana na taarifa kutoka  kwa raia wema kwamba, kulikuwepo mpango wa kuvamia Saccoss ya Msakuzi tarehe 26 Septemba 2019.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 10 Oktoba 2019 na Lazaro  Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam wakati akizungumza na wanahabari.

“Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu Dar es Salaam kupitia kikosi kazi kilichokuwa  kimeweka mtego, na ilipofika majira ya saa sita mchana zilifika pikipiki mbili aina ya boxer ambazo hazikusomeka namba zikiwa na majambazi wane.

“Mmoja kati yao akiwa na bastola, ndipo  walipoona polisi na kuanza kukimbia huku wakirushiana risasi, lakini askali mahiri walipofanikiwa kuwajeruhi wawili,” amesema.

Amesema, majeruhi hao walipopekulia, walikutwa na bastola moja, risasi tatu ndani ya magazine na maganda mawili ya risasi ambapo walipelekwa hospitali na baadaye kufariki.

“Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu, kupitia kikosi kazi chake kimefanikiwa pia kumuua jambazi hatari aliyekuwa anatafutwa kwa muda mrefu kwa kufanya matukio mbalimbali ya mauaji na ujambazi.

“Tarehe 30 Septemba 2019 saa saba mchana, Jeshi la Polisi lilipta taarifa kutoka kwa msiri wake kuwa, Ilala Boma kuna jambazi sugu anayefahamika ka jina la Emmanuel Peter maarufu kwa jina la Mark Silengo na wenzake wanne, wanapanga mipango ya kwenda kufanya uhalifu,’ amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!