Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Tume huru itasaidia kuepusha uhasama, visasi baada ya uchaguzi
Makala & UchambuziTangulizi

Tume huru itasaidia kuepusha uhasama, visasi baada ya uchaguzi

Ramadhani Kailima, Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC)
Spread the love

MJADALA juu ya umuhimu wa katiba mpya na “tume huru ya uchaguzi nchini,” bado ungali mbichi. Anaandika Saed Kubenea … (endelea).

Ubichi huu unatokana na ukweli kwamba serikali ilipuuza ushauri wa tume tatu tofauti zilizoundwa na marais Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa, na Jakaya Kikwete, kuwashauri juu ya masuala mbalimbali ya kikatiba.

Tume iliyoongozwa na Jaji Mkuu Francis Nyalali kuhoji Watanzania kama wanataka chama kimoja au vyama vingi vya siasa mwaka 1991, katika moja ya mapendekezo yake ilizungumzia umuhimu wa katiba mpya na “tume huru ya uchaguzi.”

Katika ripoti hiyo, Jaji Nyalali alitoa mifano ya nchi kadhaa ambazo zilizokuwana tume za uchaguzi zisizo huru.

Alionya kuhusu madhara yanayoweza kutokea iwapo taifa lingekosa chombo huru cha kusimamia uchaguzi. Alisema tume huru ya uchaguzi ingeweza kuepusha mauaji, machafuko, kudidimia kwa uchumi wa taifa, njaa na maradhi.

Katika ibara ya 591 ya ripoti yake, Jaji Nyalali alisisiza: “Ni lazima muundo wa tume ya taifa ya uchaguzi ubadilike, ili kukidhi haja ya demokrasia ya vyama vingi.” Hakusikilizwa.

Jaji Robert Kisanga, aliyeongoza tume ya rais ya kukusanya maoni ya wananchi kuhusu maeneo mbalimbali ya kisiasa na kiuchumi mwaka 1998, naye alitaja katiba mpya na tume huru ya uchaguzi kama moja ya mambo ya lazima.

Alisema uteuzi wa wajumbe wa tume, kwamba si sahihi wao kuteuliwa na rais – ambaye ni kiongozi wa chama cha siasa kinachotawala.

Mantiki ni kwamba kwa kuwa wengi wanaoteuliw anaye ni wafuasi wa chama wake, ama watakuwa na upendeleo kwa chama chake au watalipa fadhila kwa aliyewateuwa.

Aliseme kuwa wakati mwingine, rais anakuwa mmoja wa wagombea katika uchaguzi unaofuata. Chama chake kina wagombea kwenye nafasi mbalimbali. Hakuna shaka kuwa wasimamizi hao watajiegemeza kwenye chama cha aliyewateua. Hawakumsikiliza.

Katika mchakato wa katiba mpya ulioshinikizwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mwaka 2011, hatimaye Rais Kikwete akaunda tume ya mabadiliko ya katiba, suala hili lilijitokeza tena.

Soma makala kamili kwenye gazeti lako la SMATI la kesho Jumanne – MHARIRI

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!