Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Michezo Tulia mgeni rasmi fainali Miss Tanzania
Michezo

Tulia mgeni rasmi fainali Miss Tanzania

Spread the love

NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini, Tulia Akson atakuwa mgeni rasmi kwenye fainali ya Miss Tanzania itakayofanyika tarehe 5 Decemba, 2020 kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Waaandaji na waratibu wa tamasha hilo kupitia taarifa yao wameeleza kuwa Naibu Spika huyo amethibitisha uwepo wake kwenye tukio hilo ambao umepewa kauli mbiu ya “Urembo ni heshima”

Shindano hilo ambalo linandaliwa na kampuni The Look litakuwa na warembo 20 watakaowania taji hilo kutoka sehemu mbalimbali nchini.

Waliofanikiwa kuingia katika fainali hiyo ni Prisca Lyimo (Ubungo), Tamia Hakamu (Arusha), Juliana Rugumisa (Arusha), Yvonne Paul (Kigamboni), Ruth Benitho (Ilala), Grace Machibula (Ubungo), Rose Manfere (Temeke), Margaret Mwambi (Kigamboni), Sarafina Mageye (Kinondoni).

Wengine ni Martha Golodi (Ubungo), Zenitha Chundu (Morogoro), Deolyn Mollel (Morogoro), Hoyce Bakanoba (Tabora), Necerian Kivuyo (Dodoma), Razia Abraham (Kinondoni), Angela Pendaeli (Arusha), Advera Mwemba (Mwanza), Verynice Deokari (Kinondoni) na Gloria Fela (Ilala)

Taji hilo kwa sasa linashikiliwa na Silvia Sebastian ambaye aliwakilisha kanda ya ziwa katika shindano hilo lililofanyika 2019, alifanikiwa kuondoka na Gari na kitita cha Shilingi 10 milioni kama zawadi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!