Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Tuisenge arejea APR, asaini miaka miwili
Michezo

Tuisenge arejea APR, asaini miaka miwili

Spread the love

MSHAMBULIAJI raia wa Rwanda Jacque Tuisenge amesaini miaka miwili kuitumikia klabu ya Apr inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo akitokea klabu ya Petro Luanda ya nchini Angola. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea).

Mshambuliaji huyo ambaye aliwika na Gor Mahia ya nchini Kenya akitokea klabu ya Polisi kutoka nchini Rwanda, ameamua kurejea nyumbani mara baada ya kudumu kwa msimu mmoja na klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchini Angola.

Tuisenge ambaye ni moja ya mshambuliaji mahili kwenye ukanda wa Afrika Mashariki, amejipatia umaharufu akiwa nchini Kenya akiwa na klabu ya Gor Mahia ambayo alijiunga nayo januari 2016 akitokea nchini Rwanda na kufanikiwa kufunga jumla ya mabao 50 katika misimu minne aliyokaa hapo.

Kurejea kwake APR huenda ikaongeza chachu kwa timu hiyo katika kufanya vizuri kwenye michezo ya Ligi Kuu nchini humo na michuano ya kimataifa.

Mshambuliaji huyo alizaliwa 22 septemba, 1991 katika mji wa Gisenyi uliopo Rwanda alianza safari yake ya soka kwenye klabu ya Kiyovu Sport, na kisha kuelekea Police na baadae alifanikiwa kujiunga na Gor Mahia, 2019 alielekea nchini Angola kwenye klabu ya Petro Luanda na kurejea nyumbani kwenye klabu ya APR.  

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!